Balozi wa
Uingereza nchini Tanzania Bi. Sarah Cook Leo amemtembelea ofisini kwake Kamishna
Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na
Kupambana na dawa za kulevya Bw.
Rodgers William Siyanga na kufanya mazungumzo ya namna serikali za Uingereza
na Tanzania zitakakavyoweza kushirikiana katika kudhibiti tatizo la dawa
za kulevya . Katika ziara hiyo Balozi Cook aliambatana na maafisa kutoka ubalozi
wa Uingereza nchini Tanzania Bw.
Christopher Kiddle na Bw. Andrew Stephens.
Balozi
wa Uingereza nchini Tanzania Bi. Sarah Cook (wapili kutoka kushoto)
alipomtembelea Kamishna Jenerali wa
Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na
dawa za kulevya Bw. Rodgers William
Siyanga (wa kwanza kulia) ofisini kwake leo asubui Jijini Dar es salaam. Balozi
Cook aliambatana na maafisa kutoka ubalozi wa Uingereza nchini Tanzania Bw.
Christopher Kiddle (wa kwanza kushoto) na Bw. Andrew Stephens (wa tatu
kushoto), kutoka kulia (wapili) Makamishna wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na dawa za kulevya
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...