Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii

Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) linataraji kuwazawadia wanafunzi Saba waliofanya vizuri katika sanaa za maonyesho na uchoraji katika shule tano za sekondari nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari Mkurugenzi wa Masoko wa Basata, Vivian Shaluwa amesema kuwa wameamua kutoa zaidi tuzo ili kuongeza hamasa katika masomo ya Sanaa katika shule za Sekondari.

“Tuzo hizi zitakuwa nyenzo kwa ajili ya kujenga hamasa, ari, ubunifu na juhudi katika kuleta maendeleo kupitia masomo ya sanaa. Katika program hii wanafunzi kutoka shule 5 za sekondari zitakazohusika katika kupewa tuzo hizo, shule hizi ni Loyola, Azania za Dar es Salaam, Bukoba ya Mkoa wa Kagera, Darajani toka Mkoa wa Kilimanjaro na Arusha Sekondari toka mkoa wa Arusha.Amesema Shaluwa.

Amesema ni matarajio ya BASATA kuwa utoaji wa tuzo hizi utachochea wanafunzi wengi kusoma masomo ya sanaa, kuongeza ubunifu katika kazi za Sanaa na kuwasaidia katika kuongeza ufaulu wao darasani hasa ikizingatiwa Sanaa ni nyenzo katika kumuandaa mtoto kielimu na kimaadili.

Mkurugenzi wa Masoko wa Basata, Vivian Shaluwa Akizungumza na Waandishi wa Habri mapema leo jijini Dar es Salaam, kushoto ni Afisa Habari mkuu , Agnes Kimwanga.
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...