MACHO ya wapenzi wengi wa soka nchini wikiendi hii yatakuwa kwenye viwanja viwili nchini, lakini asilimia kubwa wanausubiria kwa hamu mtanange wa aina yake kati ya wapinzani Azam FC na Yanga, utakaofanyika kesho Jumamosi katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Jumapili vita nyingine itahamia mkoani Kagera, pale wenyeji Kagera Sugar watakapokuwa wakiikaribisha Simba katika Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba, mechi zote hizo zikitarajiwa kuamua hatima ya nafasi nne za juu kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL). 

Wakati Azam FC iliyo nafasi ya tatu kwa pointi 44 ikiwa kwenye vita kali ya kusogelea nafasi mbili za juu kileleni, inapambana na Yanga (53) ambayo ipo kwenye mchuano mkali na Simba (55) wa kuwania taji la ligi hiyo. 

Ushindi wowote wa Azam FC na Kagera Sugar, ambazo nazo zinafukuzana kuwania nafasi ya tatu, utakuwa unaziweka kwenye nafasi nzuri timu hizo kuzisogelea zaidi timu za juu na kuzitibulia mipango ya ubingwa Simba na Yanga. 

BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...