Gwiji wa siasa ya uchumi kutoka nchini Misri Profesa Samir Amin (wa pili kutoka kulia) akitoa mhadhara kuhusu 'Uwezo wa Kujitawala, Ujenzi wa Demokrasia na Ustawi wa Kijamii Afrika' katika ukumbi wa Nkurumah, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam mapema leo. Mhadhara huo uliandiliwa na Taasisi ya Uongozi kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Kutoka kushoto ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uongozi Profesa Joseph Semboja, Mwenyekiti wa Mhadhara Profesa Martha Qorro na Naibu Makamu Mkuu wa Chuo - Utafiti Profesa Cathbert Kimambo.

 Mhadhiri mstaafu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Profesa Issa Shivji akichangia katika mhadhara uliofanyika mapema leo.
 Mkusanyiko wa wanafunzi, wahadhiri na watu mbali mbali waliojitokeza kumsikiliza Profesa Samir Amin mapema leo katika ukumbi wa Nkurumah, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. 
 Mchumi mbobezi nchini Tanzania Profesa Samwel Wangwe akichangia katika mjadala.
 Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uongozi Profesa Joseph Semboja akizungumza katika mhadhara huo kwa kutoa salamu za shukrani kwa niaba ya waandaaji.

Waziri Mkuu mstaafu Mhe. Jaji Joseph Sinde Warioba ambaye pia ni Rais wa Jumuiya ya Wahitimu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Samir Amin pamoja na meza kuu wakiwa katika picha ya pamoja na uongozi wa DARUSO na UDASA kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...