KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii imeipongeza Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBA) kwa juhudi zake inazozifanya katika kuibua na kukuza vipaji vya Vijana nchini.

Pongeza hizo zimetolewa leo Wilayani Bagamoyo Mkoani Pwani na Wajumbe wa Kamati hiyo wakati walipoitembelea taasisi hiyo kwa ajili ya kukagua mradi wa ukarabati wa taasisi hiyo.

Akiongea wakati wa kikao na Watendaji wa Taasisi hiyo, Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Peter Serukamba amesema kwamba, suala la muziki, filamu na utamaduni ni suala la kipaji, hivyo halihitaji elimu kubwa kwa vijana, bali kuwepo na mazingira mazuri yatakayowezesha wenye vipaji na wasio na vipaji waweze kupata fursa ya kujifunza na kuonyesha vipaji vyao.

Mhe. Serukamba amelishauri Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA) kuweka mazuri ambayo hayatawabana vijana ambao hawakupata fursa ya elimu lakini wana vipaji, hivyo ameshauri vijana nchini wapewe fursa ya kujifunza na vipaji vyao viendelee kuibuliwa.

Sambamba na hilo, Mhe. Serukamba ameishauri taasisi hiyo kutoa elimu ya lugha mbalimbali kama vile lugha za Kiingereza, Kiswahili, Kifaransa, Kijerumani, Kichina na nyinginezo ili ziweze kuwasaidia vijana hao wawapo nje ya nchi na pindi wanapokuwa wameiva katika masomo yao ndani ya chuo hicho.

“Chuo hiki naomba kione namna ya kufundisha lugha pamoja kwamba mnafundisha muziki, basi vema mkawafundisha vijana wetu lugha mbalimbali ili waweze kwenda Duniani, kwasababu kama watakuwa na tatizo la lugha itawapa shida”, alisema Serukamba.
Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii, wakionyeshwa vifaa vitumikavyokatika uhariri wa kazi za sanaa walipoingia katika moja ya Studio ya Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBA) kujionea utendaji kazi wa taasisi hiyo, 17 Machi, 2017. 
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii, Mhe. Peter Serukamba akiongea na Wafanyakazi wa Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBA) mara baada ya kuwasili katika Taasisi hiyo kwa ajili ya kukagua mradi wa ukarabati wa taasisi hiyo, 17 Machi, 2017. 
Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii pamoja na Wafanyakazi wa Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBA) wakijadiliana wakati wa kikao 17 Machi, 2017. 
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Nape Nnauye akiongea na Wafanyakazi wa Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBA) wakati wa kikao cha kukagua mradi wa ukarabati wa taasisi hiyo, 17 Machi, 2017. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...