Kituo namba moja kwa vijana East Africa Television (EATV) Limited kikishirikiana na Taasisi ya Haki za Wanawake (HAWA foundation) kinapenda kutoa shukrani za dhati, kwa umma wa watanzania  kwa  kufanikisha kuchangia kwenye kampeni ya Namthamini.

Namthamini  ni kampeni iliyolenga katika kuchangia pedi (Taulo za Kike) kwa wanafunzi  wa Sekondari, kutokana na takwimu kuonesha karibia asilimia 45 ya wanafunzi wa kike hukosa masomo wakiwa katika hedhi kutokana na kukosa pedi za kujistiri.

Kwa wastani wanafunzi wa kike wengi hupoteza siku tano hadi saba kila mwezi kutokana na ukosefu wa pedi za kujisitiri, na kwa mwaka inakadiriwa kukosa masomo kwa takribani siku 60 hadi 70.

EATV na East Africa Radio katika kufikisha mchango wake kwa jamii, na kwa kuangalia Siku ya Wanawake Duniani, Machi mosi tuliamua kuanzisha kampeni hii kwa kuishirikisha jamii ili kumuwezesha mwanafunzi wa kike asikose masomo yake na kumfanya kutofikia lengo lake kimasomo kwa kukosa pedi pale awapo kwenye hedhi.

EATV na East Africa Radio pamoja na Taasisi ya Haki za Wanawake (Hawa Foundation) imefanikiwa kukusanya michango ya fedha taslim na pakiti za pedi zitakazowawezesha takribani wanafunzi wa kike wapatao 673 kutokukosa masomo yao kwa muda wa mwaka mzima.

Katika kampeni hii ambayo wananchi walijitokeza kuichangia katika kuonyesha kumjali mtoto wa kike aliyepo shuleni zilichangwa jumla ya shilingi 20,176,110, ambazo fedha taslim shilingi 11,774,610 na pedi za thamani ya shilingi 8,401,500.
Afisa Masoko wa East Afrika Radio Basilisa Biseko akizungumza mbele ya waandishi wa Habari (hawapo pichani),mapema leo jijini Dar,kuhusua mafanikio yaliyopatikana kupitia kampeni ya 'NAMTHAMINI',Basilisa amebainisha kuwa kupitia EATV na East Africa Radio pamoja na Taasisi ya Haki za Wanawake (Hawa Foundation) imefanikiwa kukusanya michango ya fedha taslim na pakiti za pedi zitakazowawezesha takribani wanafunzi wa kike wapatao 673 kutokukosa masomo yao kwa muda wa mwaka mzima.Pichani kulia ni Mratibu wa Vipindi Eastafrika Radio,Irene Tillya na kushoto ni Mratibu wa Vipindi EATV,Sophie Proches.
Mkurugenzi wa Taasisi ya Haki za Wanawake (HAWA) , Joyce Kiria akifafanua jambo kuhusiana na mafanikio makubwa waliyoyapata kupitia kampeni hiyo ya 'NAMTHAMINI',Kiria emesema kuwa Katika kampeni hiyo ambayo wananchi walijitokeza kuichangia katika kuonesha kumjali mtoto wa kike aliyepo shuleni zilichangwa jumla ya shilingi 20,176,110, ambazo fedha taslim shilingi 11,774,610 na pedi za thamani ya shilingi 8,401,500.
 Afisa Masoko wa East Afrika Radio Basilisa Biseko akifafanua zaidi mbele ya Waandishi wa habari (hawapo pichani),kuhusiana na mafanikio ya kampeni hiyo 'Namthamini',iliyolenga katika kuchangia pedi (Taulo za Kike) kwa wanafunzi wa Sekondari,ambapo takwimu zinaeleza kuwa karibia asilimia 45 ya wanafunzi wa kike hukosa masomo wakiwa katika hedhi kutokana na kukosa pedi za kujistiri.
 Baadhi ya Waandishi wa habari wakifuatilia mkutano huo uliofanyika mapema leo jijini Dar.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...