MAREHEMU JANUARY
CLAUDIO KISANKO
Leo
tarehe 21-Machi-2017 Baba yetu mpendwa ametimiza mwaka mmoja tangu alipoitwa na
Mwenyezi Mungu. Tunaamini yupo nasi kiroho na daima tunamshukuru Mungu kwa muda
wote aliokuwa nasi.
Misa ya
kumbukumbu itafanyika siku ya Jumamosi, Machi 25, 2017 saa mbili kamili asubuhi
katika Kanisa Katoliki la Mtakatifu Bonaventura Kinyerezi
mwisho jijini Dar es salam. Familia inawakaribisha wote siku hiyo kanisani na baadae kwenye chai
nyumbani kwa marehemu Kinyerezi mwisho.
Tunamwomba
Mungu azidi kuipumzisha Roho yake mahali pema peponi. AMINA
Raha ya
Milele umpe ee Bwana,
na Mwanga wa Milele umwangazie.
Apumzike kwa Amani. Amina
na Mwanga wa Milele umwangazie.
Apumzike kwa Amani. Amina
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...