Kaimu
Mkurugenzi Mkuu wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), Cliford Tandari
akifafanua jambo katika Mkutano wake na Baadhi ya Mabalozi
wanaoiwakilisha Tanzania nchi za nje, katika Ukumbi wa Mikutano wa Kituo
hicho, Jijini Dar es salaam leo.
Kiongozi
wa Msafara wa Mabalozi hao, Balozi wa Tanzania nchini Algeria, Balozi
Omar Yussuf Mzee akifafanua jambo katika kikao kati yao na uongozi wa
Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), walipotembelea leo ili kujionea
fursa mbalimbali za uwekezaji zinatolewa na Kituo hicho. ambapo
amewataka TIC kuhakikisha wanaandaa maeneo ya viwanda kulingana na
uzalishaji unaopatikana katika eneo husika.
Balozi
wa Tanzania nchini Korea Kusini, Matilda Masuka akizungumza jambo
katika kikao kati yao na uongozi wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC),
walipotembelea leo ili kujionea fursa mbalimbali za uwekezaji zinatolewa
na Kituo hicho.
Mkutano baina ya Baadhi ya Mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania nchi za nje na uongozi wa Kituo cha Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), wakiongozwa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu, Cliford Tandari, ukiendelea.
Balozi wa Tanzania nchini Oman, Balozi Abdallah Kilima (katikati) akizungumza katika kikao kati yao na uongozi wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC),
walipotembelea leo ili kujionea fursa mbalimbali za uwekezaji zinatolewa
na Kituo hicho.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...