Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (katikati) akizungumza
na Wawakilishi wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC)
(hawapo pichani), wakati kiongozi huyo alipokuwa anafungua Warsha iliyoandaliwa na SADC
kwa lengo la kujadili masuala mbalimbali ya usalama ndani ya Jumuiya hiyo iliyofanyika
Ukumbi wa Mikutano, Hoteli ya Ramada, jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mratibu Mkazi wa
Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez,
na Mkuu wa Kituo cha Tahadhari ya Matukio ya Kiusalama katika Sekretaireti ya SADC, Habib
Kambanga.
Mkuu wa Kituo cha Tahadhari ya Matukio ya Kiusalama katika Sekretaireti ya Jumuiya ya
Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC), Habib Kambanga akizungumza katika Warsha
iliyoandaliwa na SADC kwa lengo la kujadili masuala mbalimbali ya usalama ndani ya Jumuiya
hiyo iliyofanyika Ukumbi wa Mikutano, Hoteli ya Ramada, jijini Dar es Salaam. Mkutano huo
ulifunguliwa na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni.
Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini,
Alvaro Rodriguez (wapili kulia meza kuu) akizungumza katika Warsha iliyoandaliwa na SADC
kwa lengo la kujadili masuala mbalimbali ya usalama ndani ya Jumuiya hiyo iliyofanyika
Ukumbi wa Mikutano, Hoteli ya Ramada, jijini Dar es Salaam. Watatu kulia meza kuu ni Mgeni
rasmi Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, ambaye pia
alifungua mkutano huo.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (katikati) akisindikizwa
na Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP)
nchini, Alvaro Rodriguez (kushoto), pamoja na Mkuu wa Kituo cha Tahadhari ya Matukio ya
Kiusalama katika Sekretaireti ya Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC), Habib
Kambanga (kulia), mara baada ya Masauni kufungua Warsha ya siku mbili iliyoandaliwa na
Jumuiya hiyo ambapo Wawakilishi wa nchi wanachama wa Jumuiya hiyo walijadili masuala
mbalimbali ya usalama. Warsha hiyo ilifanyika katika Ukumbi wa Mikutano, Hoteli ya Ramada,
jijini Dar es Salaam.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...