Mshiriki wa Miss Tanzania 2014, Nargis Mohamed na Nafue Nyange wameamua kufungua shule ya urembo watakayokuwa wakitoa elimu kwa njia ya mtandao. Akizungumza jijini Dar es Salaam Nargis alisema kuwa wameamua kuandaa mafunzo hayo maalum katika fani ya urembo ili kuweza kuwawezesha wanawake na vijana waweze kujikwamua kiuchumi. 

Nargis aliongeza kuwa mafunzo hayo maalum yamewalenga watu wote na wanaweza kuyapata kidigitali, ikiwemo kwa njia ya simu au mtandao kwa gharama ya shilingi elfu kumi (10,000) tu za Kitanzania kwa mwezi. "Mafunzo hayo hayachagui jinsia; nia yetu kubwa sisi ni kuwawezesha wenzetu kwa kuwapa ujuzi ili waweze kujiinua kiuchumi kama wajasiliamali na kujijenga kimaisha sambamba na mpango wa serikali yetu kujenga ajira na kujikwamua kutoka kwenye umaskini," alisema Nargis.

 Kwa upande wake Nafue Nyange aliongeza kuwa mafunzo hayo yanapatikana kwa bei nafuu kabisa kupitia tovuti ya www.glammadamlive.com
Pia anawaomba watanzania wasajili wataweza kufanya malipo kupitia Vodacom M-pesa na Tigo Pesa. Kwa wale walio nje ya nchi wanaweza kutumia kadi tofauti kama VISA, MasterCard, American Express.
Miss Tanzania 2014, Nargis Mohamed (kushoto) akizungumza na waandishi wa habari leo nia yao ya kuanzisha darasa la urembo la kidigitali. Pembeni ni Mjasiliamali Nafue Nyange. 
Mjasiliamali Nafue Nyange akisisitiza jambo. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...