Kamishna Jenerali wa Magereza, Dkt. Juma Malewa ambaye pia ni Mlezi wa Chama cha Akiba na Mikopo cha Watumishi wa Jeshi la Magereza(TPS SACCOS LTD) akitoa maelezo mafupi kabla ya kumkaribisha Kaimu Mrajis wa Vyama vya Ushirika afungue rasmi Mkutano Mkuu wa Nne wa TPS SACCOS Ltd leo Machi 13, 2016 uliofanyika kwa siku moja katika Ukumbi wa Bwalo Kuu la Maafisa Magereza Ukonga – Dar es Salaam.
Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Tusekile Mwaisabila ambaye ni Mkuu wa Magereza Mkoa wa Lindi akitoa hoja ya kuthibitisha Notisi ya Mkutano Mkuu mbele ya Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Nne uliofanyika kwa siku moja katika Ukumbi wa Bwalo Kuu la Maafisa Magereza Ukonga – Dar es Salaam.
Kaimu Mrajis wa Vyama vya Ushirika, Bw. Colin Nyakunga akitoa salaam ya Ushirika kabla ya kutoa Hotuba ya Ufunguzi wa  Mkutano Mkuu wa Nne wa TPS SACCOS Ltd leo Machi 13, 2016 uliofanyika kwa siku moja katika Ukumbi wa Bwalo Kuu la Maafisa Magereza Ukonga – Dar es Salaam.
Wajumbe wa Mkutano Mkuu ambao ni Maafisa, Askari na Watumishi raia wa Jeshi la Magereza wenye vyeo mbalimbali ambao ni Wanachama wa TPS SACCOS LTD kutoka Mikoa yote Tanzania Bara wakisikiliza hotuba ya Mgeni rasmi katika Mkutano huo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...