Makete:
Lori lenye namba za usajili T 721 BVV lililokuwa limebeba mawe likiwa
limepinduka katika kijiji cha Masisiwe na kusababisha majeruhi na kifo
cha mtu mmoja ambaye alikuwa katika lori hilo
Taarifa za awali
kutoka eneo la tukio zinasema kuwa lori hilo lilipoteza muelekeo ghafla
kisha likaanza kupinduka kwa kubiringika mara kadhaa umbali unaokadiriwa
kuwa zaidi ya mita 80 kutoka barabarani
Ajali hiyo inadaiwa kutokea kati ya saa nane na saa tisa alasiri hii leo
Baadhi
ya mashuhuda waliokuwa eneo la tukio ambao hawakutaka kutaja majina yao
wamesema Lori hilo lilikuwa limetoka kubeba mawe kwa ajili ya kujenga
daraja katika kata ya Ipepo na likiwa njiani kueleka eneo la ujenzi
lilipopoteza muwelekeo na kupinduka kisha kuporomokea bondeni
Jeshi la polisi Makete lilifika eneo la tukio na kuuchukua mwili wa marehemu kwa uchunguzi zaidi
Tutawaletea taarifa kamili ya tukio hilo pindi mamlaka husika zitakapatia.habari/picha na Edwin Moshi wa Eddy Blog
Lori hilo linavyoonekana baada ya kupinduka.
Polisi wakipima jinsi ajali hiyo ilivyotokea.
Mwili wa marehemu ukiingizwa kwenye gari.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...