Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (wa Tatu kushoto), Mkuu wa mkoa wa Pwani, Mhandisi Evarist Ndikilo (wa kwanza kulia), Mbunge wa Chalinze, Mhe. Ridhiwani Kikwete (wa pili kulia), Mbunge wa Kibaha Vijijini, Mhe.Hamoud Jumaa (wa pili kushoto) na Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Gissima Nyamo-hanga (wa kwanza kushoto) wakifunua Jiwe la Msingi kuashiria uzinduzi wa mradi wa Usambazaji Umeme vijijini wa Awamu ya Tatu (REA III) katika mkoa wa Pwani. Hafla ya Uzinduzi huo ilifanyika katika kijiji cha Msufini mkoani humo.
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (katikati), Mkuu wa mkoa wa Pwani, Mhandisi Evarist Ndikilo (wa kwanza kushoto), Mbunge wa Chalinze, Mhe. Ridhiwani Kikwete (wa pili kushoto), Mbunge wa Kibaha Vijijini, Mhe.Hamoud Jumaa (wa nne kushoto) na Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Gissima Nyamo-hanga wakifurahia uzinduzi wa mradi wa Usambazaji Umeme vijijini wa Awamu ya Tatu (REA III) katika mkoa wa Pwani. Hafla ya Uzinduzi huo ilifanyika katika kijiji cha Msufini mkoani humo.
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo
(katikati), akikata utepe kuashiria uzinduzi wa mradi wa Usambazaji Umeme
vijijini wa Awamu ya Tatu (REA III) katika mkoa wa Pwani. Wengine katika picha
ni Mkuu wa mkoa wa Pwani, Mhandisi Evarist Ndikilo (wa kwanza kushoto), Mbunge
wa Chalinze, Mhe. Ridhiwani Kikwete (wa pili kushoto), Mbunge wa Kibaha
Vijijini, Mhe.Hamoud Jumaa (wa nne kushoto) na Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini
(REA), Mhandisi Gissima Nyamo-hanga.
Watendaji kutoka kampuni ya Steg
International Services wakimsikiliza Waziri wa Nishati na Madini (hayupo
pichani) wakati wa Uzinduzi wa Mradi wa Usambazaji Umeme Vijijini Awamu ya Tatu
katika mkoa wa Pwani. Kampuni hiyo itatekeleza sehemu ya kwanza ya Mradi huo wa
Awamu ya Tatu.
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo
(mwenye fulana ya Bluu) na Mbunge wa Chalinze, Mhe. Ridhiwani Kikwete wakifukia
nguzo ya umeme kwa udongo ikiwa ni ishara ya kuanza kwa utekelezaji wa Mradi wa
Usambazaji Umeme Vijijini, Awamu ya Tatu katika mkoa wa Pwani.
Kaimu Kamishna Msaidizi wa Nishati anayeshughulikia
Umeme, Mhandisi Salum Inegeja (wa kwanza kushoto) na Kamishna Msaidizi wa
Madini, Kanda ya Mashariki, Julius Sarota (wa pili kushoto) wakifuatilia
shughuli ya uzinduzi wa Mradi wa Usambazaji Umeme Vijijini, Awamu ya Tatu
katika mkoa wa Pwani.
Na Teresia Mhagama
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter
Muhongo, amezindua mradi wa Usambazaji Umeme
vijijini wa Awamu ya Tatu (REA III) katika mkoa wa Pwani ambao utawezesha
vijiji mbalimbali katika mkoa huo kupata huduma ya Umeme.
Hafla ya Uzinduzi huo ilifanyika katika kijiji cha
Msufini mkoani humo na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo Mkuu wa mkoa
wa Pwani, Mhandisi Evarist Ndikilo, Mbunge wa Chalinze, Mhe. Ridhiwani Kikwete
na Mbunge wa Kibaha Vijijini, Mhe.Hamoud Jumaa.
Uzinduzi wa mradi huo ulienda sambamba na utambulishaji wa Mkandarasi
atakayetekeleza sehemu ya kwanza ya Mradi huo ambaye ni kampuni ya Steg International Services.
Kupata taarifa zaidi BOFYA HAPA
Kupata taarifa zaidi BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...