Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii
JOPO la viongozi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Nchini (TFF) limeingia mchana huu kutoka Addis Ababa, Ethiopia kulipokuwa na uchaguzi mkuu wa Shirikisho la Mpira barani Afrika (CAF) uliofanyika jana.
Katika uchaguzi huo mgombea Ahmad Ahmad kutoka nchini Madagascar alimuangusha aliyekuwa rais wa Shirikisho hilko Issa Hayotou kwa kipindi cha miaka 29 kwa kura 34 kwa 20.
Rais wa TFF, amesema kuwa uchaguzi ulikuwa ni wa haki na umeonyesha mabadiliko makubwa sana katika maendeleo ya soka barani Afrika na amewaahidi wwatashirikiana nae bega kwa bega.
Kabla ya kwenda Addis Ababa, Malinzi hakuweka wazi kuwa kura yake atampa nani kwani aliamini wote ni wazuri na wanafanya kazi zao kwa uweledi mkubwa.
Waziri wa michezo wa Zanzibar, Rashid Ali Juma (pili kulia) akiwa na viongozi wa Zanzibar Football Association (ZFA) mara baada ya Zanzibar kutangazwa kuwa mwanachama wa 55 wa CAF jijini Addis Ababa, Ethiopia 
Viongozi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Nchini (TFF) wakiongozwa na Rais Jamali Malinzi (wa kwanza kulia) wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kuwasili Nchini kutokea Addis Ababa, Ethiopia kwenye uchaguzi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu barani Afrika (CAF).
 Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Nchini (TFF) akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kuwsili uwanja wa ndege kutoka Addis Ababa Ethiopia kulipokuwa na uchaguzi Shirikisho la Mpira wa Miguu barani Afrika (CAF).
  Mwenyekiti wa zamani wa Chama cha soka cha Mpira (FAT) na mjumbe wa heshima wa  Shirikisho la Mpira wa Miguu barani Afrika (CAF) Said El maamury  akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kuwsili uwanja wa ndege kutoka Addis Ababa Ethiopia kulipokuwa na uchaguzi Shirikisho hilo.




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...