Mkuu wa Mkoa Paul Makonda akizungumza mbele ya wageni waalikwa mbalimbali,wakiwemo Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa jiji la Dar,viongozi wa Dini mbalimbali,Wasaniii na vijana kutoka vituo mbalimbali vya matibabu ya dawa za kulevya walijitokeza kumsikiliza RC Paul Makonda ambaye leo alikuwa anatimiza mwaka wake mmoja wa Uongozi tangu aapishwe na Rais wa awamu ya tano,Dkt John Pombe Magufuli.
Baadhi ya waathirika wa Madawa ya Kulevya wapato zaidi ya 1500 kutoka vituo mbalimbali vinavyotoa matibabu ya Dawa za kulevya,wakiwa ndani ya bwalo la Polisi Oysterbay jijini Dar,wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa Paul Makonda alipokuwa akizungumza nao mambo mbalimbali,ya kimaendeleo pamoja na kupewa elimu mbalimbali ihusuyo dawa za kulevya.RC Makonda leo anatimiza mwaka mmoja tangu aapishwe kuwa mkuu wa mkoa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt John Pombe Magufuli,
Baadhi ya Viongozi mbalimbali wa dini,walialikwa kwenye hafla hiyo fupi ya kutimiza mwaka mmoja kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar,Paul Makonda
Pichani ni baadhi ya wasanii walioshiriki na kutoa neno katika hafla hiyo,wasanii hao ni TID,Diamond Paltnumz,Harmonize,Banana Zorro,Mrisho Mpoto na wengineo ambao walijitokeza kumuunga mkono RC Makonda katika suala zima la kupambana na Dawa 
za kulevya.

Vijana waliothiriwa na Madawa ya kulevya ambao kwa sasa wameahidi kuacha kutumia wakiwa wameandika bango lao la kumshukuru RC Makonda kwa kazi yake nzuri aifanyayo ya kupambana na Dawa za Kulevya.
Vijana mbalimbali walikokuwa wakitumia dawa za kulevya wakimshukuru RC Makonda kwa juhudi zake kubwa za kuhakikisha dawa za kulevya zinatokomezwa ndani ya jiji la Dar kwa namna moja ama nyingine

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...