Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii
Timu ya Taifa ya vijana chini ya miaka 17 Serengeti Boys imepangwa  Kundi B katika Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika kwa vijana chini ya umri wa miaka 17, zitakazofanyika nchini Gabon kuanzia Mei 14 hadi 28, mwaka huu.
Serengeti walifuzu kuingia katika fainali hizo baada ya kushinda rufaa yao dhidi ya Congo Brazaville kushindwa kumpeleka mchezaji wao aliyechezeshwa kwenye kikosi cha vijana lakini akisadikiwa kuwa ni mkubwa kiumri tofauti na kanuni za mashindano hayo. 
Congo Brazaville walishindwa kumuwasilisha kwa vipimo zaidi ya mara tatu walipohitajiwa na CAF na hivyo CAF kuamua kuwaondoa kwenye nafasi hiyo na kuchukuliwa na Tanzania..
Kundi B, Serengeti Boys wamepangwa na Angola, Niger na Mali ambapo kwa sasa Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani (FIFA) limewafungia baada ya Serikali ya nchi hiyo kuingilia masuala ya soka na  kuwafukuza viongozi wa Shirikisho la Soka la nchi hiyo (FEMAFOOT).  
Kundi A lina timu za wenyeji Gabon, Guinea, Cameroon na Ghana na ikumbukwe timu mbili za juu kila kundi zitafuzu moja kwa moja Fainali za Kombe la Dunia za U-17 nchini India baadaye mwaka huu.

Awali  fainali hizo zilitakuwa kufanyika nchini Madagascar lakini Gabon aliyekuwa rais wa  Shirikisho la Soka Afrika (CAF)  Issa Hayatou wa Cameroon alisema  nchi hiyo haikukidhi vigezo vya kuandaa mashindano hayo.
Kikosi cha timu ya Tifa ya vijana chini ya miaka 17 Serengeti Boys.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...