Mashirika na asasi zote ambazo hazikumbatii na kukubali mfumo wa kuendesha biashara kidigitali zinajiweka pabaya kutemwa na wateja wao.

Kutokana na tishio hili, Telkom and Business Connexion inazindua rasmi BCX, mfumo mpya na wa kisasa kidigitali unaoongoza barani Afrika, unaotumika kurahisisha mawasiliano ya miamala ya biashara na mawasiliano.

Toleo hili jipya la teknolojia, lililoandaliwa kwa ushirika kati ya Telkom Business na Business Connexion, ni la kipekee katika ufumbuzi wa kitekinolojia unaosambaa kwa kasi barani Afrika kuwezesha na kurahisisha mawasiliano na ufanisi wa kibiashara.

“Uzinduzi wa BCX kwa kweli unafungua ukurasa mpya katika mwelekeo wa ufanisi wa kibiashara kwa tekinoljia pevu barani Afrika,” alisema Seronga Wangwe ambaye ni Mkurugenzi wa BCX Tanzania, katika hotuba yake ya ufunguzi aliyoitoa hoteli ya Kilimanjaro Hyatt Regency, jijini Dar Es Salaam.

“BCX imejengwa kutoka katika msingi imara wa Telkom Business yenye maarifa na elimu pevu ya miundombinu ya mawasiliano pamoja na taaluma ya muunganisho wa kibiashara inayojali kutoa huduma kwa ukaribu na unyenyekevu kwa wateja wake.

“BCX sasa ni bidhaa mpya ya mawasiliano barani Afrika yenye ufanisi wa kutoa huduma kwa umakini mkubwa’, aliongeza Bwana Wangwe.

Mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya BCX Tanzania Bw. Seronga Wangwe (kushoto) akizungumza na waandishi wa habari Dar es salaam katika uzinduzi wa kampuni ya BCX ambayo imejumuisha kampuni za Business connexion na Telkom katika hafla fupi iliyofanyika katika hoteli ya Hyatt Regency, Kulia ni meneja mauzo wa kampuni hiyo Bw. Ebenezer Massawe.

Kutoka kushoto ni Bwa. Seronga Wangwe, (mwakilishi) kutoka Mozambique High Commission, Bwa.Frans Van Aardt- Councelor kutoka ubalozi wa Afrika kusin,Bi.Monica Patricio Clemente- Balozi wa Msumbiji, pamoja na Bwa.Althon Beukes- mkuu wa BCX International wakiwa katika picha ya pamoja.

. Mgeni rasmi Bw. Frans Van Aardt ambaye ni Councelor wa Ubalozi wa Afrika Kusini nchini Tanzania. Akizungumza katika Uzinduzi wa kampuni ya BCX uliofanyika Hyatt hotel Dar es salaam
Mkuu wa BCX International Bw. Althon Beukes akizungumza na wageni katika hafla fupi ya uzinduzi wa kampuni ya BCX, iliyofanyika katika hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es salaam
Wageni mbalimbali waliohudhuria katika hafla ya uzinduzi wa BCX Tanzania .

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...