Tanzania, Sio Salama kabisa Kimtandao na kumekua na matukio kadhaa ya kujaribu kushambulia TRA pamoja na mashirika mengine.

Tanzania, Ambapo imeendelea kuonekana ikikusanya pesa nyingi - Imekua ikiangaziwa macho na wahalifu Mtandao.

Binafsi, Nimesha chukua hatua kadhaa ya kukutana na TRA kuhusiana na matishio ya kimtandao - Na walikiri kupokea mashambulizi mengi huku wakisema wamechukua hatua za kuwasilisha malalamiko eGA.

Niliwashauri washirikishe vitengo vingine kama TZ-CERT na CYBERCRIME UNIT paamoja na wadau wengine ili kuhakiki wanakomesha majaribio hayo ya kihalifu kimtandao ambayo yanaweza kuligharimu Taifa na kusababisha Hasara kubwa.

Itakumbukwa hivi karibuni, Waziri Mkuu Mh. Majaliwa, Alizungumzia swala la uhalifu mtandao katika Shirika la Ndenge Tanzania.

Naendelea kutoa wito, Tufunge mikanda ili tuweze kuwabaini wahalifu Mtandao pamoja na kuwachukulia hatua stahiki

Kenya, wameonyesha nia ya kukabiliana na hali hii kwa dhati na Tanzania tuongeze nguvu.
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...