Na Chalila Kibuda , Globu ya Jamii
Wananchi wa Mkuranga wametakiwa kujitokeza kupima magonjwa mbalimbali na pale wanapokutwa kuweza kutibu kwa wakati mwafaka.
Akizungumza
katika upimaji wa Afya huo,Mkurugenzi wa Taasisi ya Ibun Jazar na
Mwenyekiti wa Jumuiya kuhifadhisha Qur-uan Tanzania, Othman Kaporo
amesema kuwa katika dunia ya sasa jamii inawajibu wa kupima afya kujua
ana tatizo au hana ili kuweza kuchukua hatua pamoja na kujinga na
magonjwa mbalimbali yanatokana na mfumo wa maisha.
Othman amesema
kuwa huduma hiyo itatolewa kwa wa wananchi wa Mkuranga, Vikindu,
Mwanambaya, Mbagala na maeneo mengine yaliyo karibu.
Amesema
wamechagua Wilaya hiyo kutokana watu wengi wanashindwa kuifikia na kuona
kwa taasisi hiyo inawajibu wa kupima afya za wananchi ha.
Aidha
amesema kuwa watu wengine ambao wanauwezo wajitokeze katika kutoa huduma
ya upimaji ili waweze kujikinga na magonjwa ambayo yanatokana na mfumo
wa maisha.
Amesema tangu jana walipoanza kupima watu zaidi ya 500
wamwjitokeza kupima na mwitikio umekuwa mkubwa wa kuweza kuvuka malengo
ya upimaji huo.
Huduma ya vipimo walivyotoa ni Msukumo wa Damu (BP),
Sukari , Unene na Urefu kuendana sawa na mwili (BMI) Ushauri Nasaha na
Upimaji wa VVU,Utafiti wa Saratani ya matiti pamoja na utafiti wa
Saratani ya Kizazi.
Mkurugenzi wa Taasisi ya Ibun Jazar na Mwenyekiti wa Jumuiya kuhifadhisha Qur-uan Tanzania, Othman Kaporo akizungumza na waandishi habari (hawapo pichani) wakati wa upimaji wa afya kwa wananchi wa Wilaya ya Mkuranga leo.
Muuguzi Mariam Adamu akipima kipimo cha Sukari na Msukumo wa Damu
Wananchi wakisubiri huduma ya vipimo vinavyotolewa na Taasisi ya Ibun Jazar leo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...