Waziri  wa Maji na Umwagiliaji wa Tanzania  Gerson Lwenge ameishukuru Kuwait kwa kusaidia miradi mbalimbali ya maji inayotekelezwa hapa nchi na kueleza kuna anatarajia ushirikiano zaidi hasa katika miradi ya umwagiliaji. 

Kupitia mikopo mbalimbali inayotolewa  na Mfuko Wa Kuwait Wa Maendeleo ya Kiuchumi kwa miradi mikubwa ya umwagiliaji. 

Waziri Lwenge alitolea mfano wa mradi wa hivi karibuni katika mikoa ya Same na Mwanga, Kaskazini  mwa Tanzania, mradi ambao una thamani ya dola za marekani milioni 34.

Waziri pia aligusia miradi mingine miwili  ya umwagiliaji katika  bonde la Muhongo na Luichi kaskazini-magharibi mwa Tanzania ambayo ina thamani ya dola za marekani milioni 15. 

Mfuko wa Maendeleo wa Kuwait unatarajia kutuma wataalamu wake Tanzania kwa  lengo la kutathmini miradi hii  miwili katika nusu ya kwanza ya mwaka 2018. 

 Waziri pia alitoa Pongezi na shukrani zake za dhati kwa ujumbe wa Kuwait Red Crescent Society uliofanya ziara nchini Tanzania hivi karibuni na kufungua visima 16 katika shule mbalimbali  za serikali ikiwa ni utekelezaji wa Mpango wa Kisima kwa Kila Shule.

Ikumbukwe kuwa Balozi wa Kuwait nchini Tanzania Mhe. Jassim Al Najema ameanzisha  mpango huo wa Kisima kwa Kila Shule kuunga mkono wito wa Rais John Magufuli wa kusaidia sekta ya elimu nchini na kukabiliana na ukame na uhaba wa maji safi ya kunywa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...