Balozi wa Tanzania nchini Uingereza na Ireland, Dkt Asha-Rose Migiro mapema mwezi huu aliwasilisha hati ya utambulisho (letter of credence) kwa Rais wa Ireland, Mhe. Michael D. Higgins.
Akiwasilisha hati hiyo katika Ikulu ya Ireland, Balozi Migiro alimfikishia Rais Higgins salam za Mhe. Rais John Magufuli na wananchi wa Tanzania pamoja na kumuahidi kufanya kazi itakayoimraisha uhusiano wa kihistoria baina ya Serikali za Tanzania na Ireland pamoja na kuanzisha maeneo mapya ya ushirikiano kwa kuzingatia vipaumbele vya Serikali ya awamu ya tano ya kujenga uchumi wa viwanda. Kabla ya kuagana na Rais Higgins, Balozi Migiro alikagua gwaride rasmi liliondaliwa na kikosi cha Jeshi la Anga la nchi hiyo.  
Akiwa Ireland, Balozi Migiro pia alikutana kwa mazungumzo na wanadiaspora wa Tanzania waishio katika miji mbalimbali ya Ireland.
Katika mkutano huo aliwasihi wanadiaspora kushikamana, kuwa wamoja na kuunda Jumuiya ya Watanzania waishio Ireland akiwakumbusha kauli ya wahenga isimayo kuwa 'Umoja ni nguvu, utengano ni udhaifu'.
Balozi wa Tanzania nchini Uingereza na Ireland, Dkt Asha-Rose Migiro  akimkabidhi Rais Michael D. Higgins hati ya utambulisho kutoka kwa Mhe.Rais John Pombe Magufuli.
Balozi wa Tanzania nchini Uingereza na Ireland, Dkt Asha-Rose Migiro  akikagua gwaride la heshima la kikosi cha jeshi la anga la Ireland
Balozi wa Tanzania nchini Uingereza na Ireland, Dkt Asha-Rose Migiro  akiagana na Rais Higgins.
 Michael D. Higgins akimuaga Balozi wa Tanzania nchini Uingereza na Ireland, Dkt Asha-Rose Migiro baada ya kupokea hati yake ya utambulisho 
Balozi wa Tanzania nchini Uingereza na Ireland, Dkt Asha-Rose Migiro  alikutana kwa mazungumzo na wanadiaspora wa Tanzania waishio katika miji mbalimbali ya Ireland.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...