Balozi mpya wa Tanzania nchini Kenya, Mheshimiwa Dkt. Pindi Hazara Chana ameripoti kwenye kituo chake cha kazi jijini Nairobi na kulakiwa na wafanyakazi wa kituo hicho.
Balozi Chana amekutana na wafanyakazi wa kutoka nyumbani na wale walioajiriwa hapa Kenya. Balozi ameelezea kituo cha Nairobi kama moja ya vituo vyenye shughuli nyingi na vinavyosifiwa kwa utendaji mzuri licha ya mazingira magumu ya kazi. Amewaahidi wafanyakazi kuwa atakuwa kiongozi wa kujichanganya kwani anaamini katika uwazi, umoja na mshikamano kazini.
"Nitajichanganya sana na ninyi kwa sababu nimetumwa kuwatumikia watu. Sera yangu ya kazi ni uwazi, upendo na mshikamano. Tufanye kazi kama familia moja," alisema.
Balozi Chana amesema Kenya ni jirani mwema wa Tanzania na nchi hizo zina historia ndefu ya undugu na ushirikiano, hivyo kazi yake ni kuhakikisha ushirikiano huo unaimarishwa na kudumishwa.
 Balozi Chana akikaribishwa kwenye ofisi za Ubalozi na Mwambata wa Utawala, Bi Aneth Mmari
 Balozi akisalimiana na wafanyakazi wa Ubalozi. Wa kwanza kulia ni Konseli Mkuu wa Tanzania Mombasa, Mheshimiwa Khalifan Shehe Saleh
 Balozi Chana akisalimiana na wafanyakazi wa Ubalozi waliojipanga kumlaki.
Balozi Chana akiongea na wafanyakazi wa Ubalozi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...