Mwambata Jeshi wa
Israel Barani Afrika Bw. Aviezer Segal akionesha michoro ya muundo wa Ofisi
yake wakati wa ziara ya Balozi wa Israel Mhe. Yahel Vilan alipotembelea Idara
ya Maafa ili kuangalia eneo lililotengwa kwaajili
ya Ujenzi wa Kituo cha Kitaifa na Kimataifa cha Operesheni na Mawasiliano ya
Dharura, Dodoma.
Mratibu wa Maafa
Idara ya Uratibu wa Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu Bw.Charles Msangi akionesha
muundo wa Idara hiyo wakati wa ziara ya ya Balozi wa Israel Mhe. Yahel Vilan
katika Ukumbi wa Mikutano Ofisi ya Waziri Mkuu Dodoma Aprili 4, 2017.
Katibu Mkuu Ofisi ya
Waziri Mkuu (Sera na Uratibu) Dkt. Hamisi Mwinyimvua (wa kwanza mwenye miwani)
akifuatilia mada ya muundo wa Idara ya Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu wakati wa
Ziara ya Balozi wa Israel Mhe. Yahel Vilan Dodoma.
Waziri Nishati na
Madini, Prof. Sospeter Muhongo (wa pili kutoka kushoto) akizungumza na baadhi
wa wageni walioambatana na Balozi wa Israel Mhe. Yahel Vilan alipotembelea
Idara ya Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu Aprili 4, 2017 Dodoma.
Mkurugenzi wa Idaya
ya Uratibu wa Maafa Ofisi ya Waziri Brig. Jenerali, Mbazi Msuya
(wa kwanza kushoto) akimuonesha Balozi wa Israel Mhe. Yahel Vilan ramani ya eneo lililotengwa kwaajili ya Ujenzi wa Kituo
cha Kitaifa na Kimataifa cha Operesheni na Mawasiliano ya Dharura, Dodoma.
Katibu Mkuu Ofisi ya
Waziri Mkuu (Sera na Uratibu) Dkt. Hamisi Mwinyimvua (katikati waliokaa) akiwa
katika picha ya pamoja na viongozi na baadhi ya Watendaji wa Serikali
walioshiriki katika ziara ya Balozi wa Israel Mhe. Yahel Vilan mara baada ya
kumpokea Ofisi ya Waziri Mkuu Dodoma.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...