Mkurugenzi wa Wateja Wakubwa na Serikali wa NMB –Richard Makungwa (kulia) akimpongeza mwenyekiti wa jukwaa la wahariri TEF- Teophil Makungwa mara baada ya kupokea mfano wa hundi yenye thamani ya shilingi milioni ishirini kutoka benki ya NMB. NMB imetoa kiasi cha fedha hiyo kama sehemu ya ufadhili wa mkutano wa mwaka wa jukwaa la wahariri ambao umefanyika mkoa wa Kilimanjaro. Wengine katika picha ni maofisa wa benki wakishuhudia tukio hililililofanyika mwishoni mwa wiki hapa Kilimanjaro. Baadhi ya Wajumbe wa Mkutano wa mwaka wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) wakizungumza katika mkutano huo uliofanyika Mkoa wa Kilimanjaro. Wengine katika picha ni maofisa wa benki wakishuhudia tukio hililililofanyika mwishoni mwa wiki hapa Kilimanjaro. Benki ya NMB imetoa kiasi cha sh 20,000 kama sehemu ya ufadhili wa mkutano huo. Baadhi ya Wajumbe wa Mkutano wa mwaka wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) wakizungumza katika mkutano huo uliofanyika Mkoa wa Kilimanjaro. Wengine katika picha ni maofisa wa benki wakishuhudia tukio hililililofanyika mwishoni mwa wiki hapa Kilimanjaro. Benki ya NMB imetoa kiasi cha sh 20,000 kama sehemu ya ufadhili wa mkutano huo.

BENKI ya NMB imedhamini mkutano mkuu wa mwaka wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) uliofanyika kwa siku moja ya Aprili 4, 2017 mkoani Kilimanjaro na kuhudhuriwa na wahariri wa vyombo mbalimbali nchini ambao ni wanachama wa TEF. 

Akizungumza katika uzinduzi wa mkutano huo, Afisa Mkuu wa Wateja Wakubwa na Serikali, Richard Makungwa alisema NMB inathamini mchango wa waandishi wa habari nchini na imekuwa ikishikiana nao kwa muda mrefu hivyo kudhamini mkutano huo ni sehemu ya kuendeleza ushirikiano ulipo baina ya NMB na waandishi wa habari. 

“Kwa niaba ya uongozi wa Benki ya NMB, napenda kuchukua nafasi hii kuwapongeza kwa dhati kabisa kwa kutambua kuwa NMB ni benki iliyo karibu na jamii yote ya Watanzania na kugusa mahitaji ya kila jamii ya watanzania wa kila kada. 

“Waandishi wa habari kwa NMB ni wadau muhimu sana kwani mafanikio ya NMB mpaka kufikia hapa kwa kiasi kikubwa yamechangiwa na vyombo vya habari. Hivyo tunafarijika na sisi kushikiriana nanyi kwenye shughuli zinazowagusa ninyi moja kwa moja,” alisema Makungwa na kuongeza.

 “Kwa NMB, huu ni mkutano muhimu sana na maazimio mtakayoyafikia, yatakuwa yenye tija huku mkiweka mbele uzalendo wan chi yetu. Mkiwa mnaendelea na mkutano huu, tambueni kuwa tunawathamini sana na kazi zenu tunazithamini sana.” 

Udhamini wa NMB kwa mkutano mkuu wa mwaka wa TEF una thamani ya milioni 20 na hiyo siyo mara ya kwanza kwani hata mwaka jana ilidhamini mkutano wa TEF, mkutano mkuu wa mwaka wa TBN, mkutano wa TAJATI na pia NMB kuwezesha kutolewa kwa tuzo za uandishi mahiri kwa kushirikiana na MCT.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...