Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

Shirikisho la mMpira wa Miguu Nchini (TFF) limewaomba watanzania na wadau wa mpira kuichangia timu ya vijana chini ya miaka 17 Serengeti Boys ili kuiwezesha kuweka kambi ya mwezi mmoja nchini Moroco.

Serengeti Boys wameondoka nchini jana saa 8 mchana kueleka nchini Moroco kwa ajili ya kambi kabla ya kuelekea Gabon kwa ajili ya fainali za vijana zitakazoanza Mei 14.

Kabla ya kwenda Gabon, Serengeti inatarajiwa kucheza mechi mbili za kirafiki kwa ajili ya maandalizi zaidi ya kujipima na wamepangwa kundi B wakiwa na mabingwa watetezi wa kombe hilo Mali.

Timu mbili za juu za kila kundi zitawakilisha Afrika katika fainali za Kombe la Dunia nchini India 

Kauli mbiu 

Gabon mpaka kombe la Dunia...........................

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...