Mkuu wa Wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma, Cosms Nshenye akiwaonesha waandishi wa habari hawapo pichani mashina ya bangi yaliyolimwa katika shamba la mkulima wa kijiji cha Liweta ambaye hakufahamika jina lake walipokuwa katika msakao wa kuyabaini na kuteketeza mashamba ya Bangi.
Baadhi ya Askari Polisi kutoka kituo kikuu cha Polisi Wilayani Songea wakindelea na kazi ya kung'oa bangi katika moja ya shamba katika kijiji cha liweta katika halmashauri ya Wilaya ya Songea mkoni Ruvuma, halmashauri hiyo ni miongoni mwa halmashauri ambazo wananchi wamekithiri katika kilimo hicho.
Afisa Masoko wa Kampuni ya Pannar Seed (T) ltd, Sabasaba Manase akiwaonesha wakulima wa kijiji cha mletele katika manispaa ya songea mkoani Ruvuma shamba lililotumia mbegu aina ya pan 15 zinazosambazwa na kampuni hiyo.mbegu hizo zinatajwa kuleta mafanikio makubwa kwa wakulima kutokana na kukomaa haraka,kujaa vizuri na hata kuhimili hali ya hewa ikilinganishwa na mbegu za makampuni mengine.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...