Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt Medard Kalemani (wa pili kutoka
kulia), akifunua kitambaa kilichofunika Jiwe la Msingi, kuashiria uzinduzi
rasmi wa Mradi Kabambe wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya
Tatu (REA III), kwa Mkoa wa Shinyanga. Wanaoshuhudia kutoka
kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA),
Mhandisi Gissima Nyamo-Hanga, Mwenyekiti wa Wabunge wa Mkoa wa
Shinyanga ambaye pia ni Mbunge wa Msalala, Ezekiel Maige na
Mbunge wa Kishapu, Seleman Nchambi.
Na Veronica Simba – Shinyanga
Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt. Medard Kalemani, amemtaka
Mkandarasi kutoka Kampuni ya M/s OK Electronics and Electric Limited,
atakayetekeleza kazi ya kusambaza umeme vijijini Awamu ya Tatu (REA
III) kwa Mkoa wa Shinyanga, kuhakikisha anaajiri wananchi wenye sifa
kutoka maeneo hayo badala ya kuleta wafanyakazi kutoka mbali.
Alitoa maagizo hayo hivi karibuni katika Kijiji cha Negezi, wilayani
Kishapu, Mkoa wa Shinyanga, wakati wa hafla ya uzinduzi wa Mradi
Kabambe wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya Tatu (REA III) kwa
Mkoa huo.
Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt Medard Kalemani, akiwahutubia wananchi wa Kijiji cha Negezi, Wilaya ya Kishapu (hawako pichani), wakati wa uzinduzi wa Mradi Kabambe wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya Tatu (REA III), kwa Mkoa wa Shinyanga. Uzinduzi huo ulifanyika hivi karibuni.
“Tumia wataalam/vibarua vijana kutoka maeneo haya. Hatutapenda
uajiri watu kutoka mbali wakati wafanyakazi wenye sifa wako
hapahapa,” alisema Naibu Waziri.
Aidha, Dkt. Kalemani, alimwagiza Mkandarasi huyo kuhakikisha
anawalipa vibarua mara moja kila wanapokamilisha kazi husika.
“Hakuna kulaza malipo kwa sababu sisi tunakulipa vizuri.”
Sambamba na maagizo hayo, Dkt Kalemani, aliutaka uongozi wa Shirika
la Umeme Tanzania (TANESCO) mkoani humo, kujipanga na
kumsimamia Mkandarasi husika ili kuhakikisha anafanya kazi masaa 24
kwa siku.
Alisisitiza kuwa, Ofisa yeyote atakayelegalega kumsimamia Mkandarasi
husika kadri inavyotakiwa. Atawajibishwa kwa kuondolewa katika nafasi
yake.
Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt Medard Kalemani, akiwatunza na kujumuika kucheza ngoma pamoja na moja ya vikundi vya burudani kutoka Shinyanga, kilichokuwa kikitumbuiza wakati wa hafla ya uzinduzi wa Mradi Kabambe wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya Tatu (REA III), kwa Mkoa wa Shinyanga hivi karibuni.
BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI
BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...