Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt Medard Kalemani (wa pili kutoka kulia), akifunua kitambaa kilichofunika Jiwe la Msingi, kuashiria uzinduzi rasmi wa Mradi Kabambe wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya Tatu (REA III), kwa Mkoa wa Shinyanga. Wanaoshuhudia kutoka kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Gissima Nyamo-Hanga, Mwenyekiti wa Wabunge wa Mkoa wa Shinyanga ambaye pia ni Mbunge wa Msalala, Ezekiel Maige na Mbunge wa Kishapu, Seleman Nchambi.

Na Veronica Simba – Shinyanga

Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt. Medard Kalemani, amemtaka Mkandarasi kutoka Kampuni ya M/s OK Electronics and Electric Limited, atakayetekeleza kazi ya kusambaza umeme vijijini Awamu ya Tatu (REA III) kwa Mkoa wa Shinyanga, kuhakikisha anaajiri wananchi wenye sifa kutoka maeneo hayo badala ya kuleta wafanyakazi kutoka mbali.

Alitoa maagizo hayo hivi karibuni katika Kijiji cha Negezi, wilayani Kishapu, Mkoa wa Shinyanga, wakati wa hafla ya uzinduzi wa Mradi Kabambe wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya Tatu (REA III) kwa Mkoa huo.
Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt Medard Kalemani, akiwahutubia wananchi wa Kijiji cha Negezi, Wilaya ya Kishapu (hawako pichani), wakati wa uzinduzi wa Mradi Kabambe wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya Tatu (REA III), kwa Mkoa wa Shinyanga. Uzinduzi huo ulifanyika hivi karibuni.

“Tumia wataalam/vibarua vijana kutoka maeneo haya. Hatutapenda uajiri watu kutoka mbali wakati wafanyakazi wenye sifa wako hapahapa,” alisema Naibu Waziri. Aidha, Dkt. Kalemani, alimwagiza Mkandarasi huyo kuhakikisha anawalipa vibarua mara moja kila wanapokamilisha kazi husika. “Hakuna kulaza malipo kwa sababu sisi tunakulipa vizuri.”

Sambamba na maagizo hayo, Dkt Kalemani, aliutaka uongozi wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) mkoani humo, kujipanga na kumsimamia Mkandarasi husika ili kuhakikisha anafanya kazi masaa 24 kwa siku. Alisisitiza kuwa, Ofisa yeyote atakayelegalega kumsimamia Mkandarasi husika kadri inavyotakiwa. Atawajibishwa kwa kuondolewa katika nafasi yake.
Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt Medard Kalemani, akiwatunza na kujumuika kucheza ngoma pamoja na moja ya vikundi vya burudani kutoka Shinyanga, kilichokuwa kikitumbuiza wakati wa hafla ya uzinduzi wa Mradi Kabambe wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya Tatu (REA III), kwa Mkoa wa Shinyanga hivi karibuni.

BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...