UPATIKANAJI wa huduma za Benki ya NMB umezidi kuboreshwa na sasa umesogezwa zaidi mtaani kwako. Mteja wa NMB na asiyekuwa mteja kupitia huduma ya NMB Wakala sasa anaweza kuweka kutoa fedha na hata kulipia huduma mbalimbali akiwa mtaani kwake bila ya uhitaji wa kufika katika tawi la benki ya NMB. 

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam na waandishi wa habari alipokuwa akitambulisha huduma hiyo iliyoboreshwa zaidi, Mkuu wa Idara ya Huduma Mbadala za Kibenki wa NMB, George Kivaria alisema kuboreshwa kwa huduma hiyo sasa kunawawezesha wateja kupata huduma za benki hiyo kwa haraka na kwa usalama na uhakika popote walipo.

Alisema huduma hiyo pia inamwezesha mteja wa NMB kuweza kuweka fedha, kutoa, kujua salio lake kwa gharama nafuu zaidi, huku ikitolewa na mawakala zaidi ya 2000 ambao wanapatikana maeneo mbalimbali ya nchi ikiwemo maeneo ya vijijini. 

Alisema lengo la NMB ni kusogeza huduma zake karibu zaidi na wateja ili kurahisisha upatikanaji wa huduma zake tena kwa gharama nafuu. Alisema huduma zingine ambazo wateja wengine hata wasiokuwa na akaunti za NMB wanaweza kufanya kwa mawakala hao ni pamoja na kulipa ada za shule, kulipia tozo za luku, ving'amuzi, malipo ya TRA, leseni na bili za maji.
Meneja Uwakala wa Benki ya NMB, James Wanyama (kulia) akifafanua jambo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) walipokuwa wakizinduwa huduma za NMB Wakala zilizoboreshwa zaidi zenye gharama nafuu. Kushoto ni Mkuu wa Idara ya Huduma Mbadala za Kibenki wa NMB, George Kivaria. Kwa huduma hizo mteja wa NMB anaweza kuweka na kutoa fedha mtaani kwake, kuangalia salio na hata kufanya malipo ya tozo mbalimbali akiwa katika mawakala wa NMB popote alipo.
Mkuu wa Idara ya Huduma Mbadala za Kibenki wa NMB, George Kivaria (kushoto) akizungumza na waandishi wa habari leo Makao Makuu ya Benki hiyo jijini Dar es Salaam alipokuwa akizinduwa huduma za NMB Wakala zilizoboreshwa zaidi. Kulia ni Meneja Uwakala wa Benki ya NMB, James Wanyama.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...