Na
Lydia Churi-MAHAKAMA, ARUSHA
Jaji Kiongozi wa
Mahakama Kuu ya Tanzania Mheshimiwa Ferdinand Wambali amewataka Majaji wa
Mahakama Kuu nchini kufanya kazi zao kwa kuzingatia Maadili, kuwa waaaminifu na
kushirikiana katika kuwahudumia wananchi ili kesi zimalizike kwa haraka katika
Mahakama mbalimbali.
Akifungua Mafunzo ya
siku tano ya Majaji wa Mahakama Kuu ya Tazania kuhusu Uongozi katika shughuli
za Mahakama leo jijini Arusha, Jaji
Kiongozi amesema lengo la Mafunzo hayo ni kujadiliana kwa kina nini kifanyike
ili kesi zimalizike mapema kwenye mahakama mbalimbali nchini.
Jaji Wambali alisema katika mkutano huo, Majaji
watapata nafasi ya kujifunza Mpango Mkakati wa Miaka Mitano wa Mahakama ya
Tanzania wenye nguzo tatu ambazo ni pamoja na masuala ya Utawala, Upatikanaji
wa haki kwa wakati na imani ya wananchi kwa Mahakama na ushirikishwaji wa wadau
katika shughuli za Mahakama.
Katika Mafunzo hayo pia
Majaji watajadiliana ni nini kilifanyika mwaka jana katika umalizwaji wa
mashauri, changamoto zilizojitokeza na nini kifanyike ili kutatua changamoto
zinazojitokeza katika utendaji wao wa kazi wa kila siku.
Naye
Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania Mheshimiwa Katarina Revokati
akizungumza na Waandishi wa habari kabla ya kuanza kwa mafunzo hayo alisema
yamegawanyika katika makundi matatu ambapo kundi la kwanza ni la Majaji
wa Mahakama ya Rufani, kundi la pili ni la Majaji Wafawidhi
wa Kanda 14 za Mahakama Kuu ya Tanzania na kundi la Tatu ni la Majaji wengine wote.
Alisema Majai wa
Mahakama ya Rufani watapatiwa Mafunzo kuhusu namna ya kutoa maamuzi ya Mahakama
katika usikilizwaji wa kesi ngazi ya Rufaa, ambapo Majaji Wafawidhi watapewa
mafunzo kuhusu Usimamizi wa uendeshaji wa kesi wakati Majaji wengine watapatiwa
mafunzo kuhusu uongozi na usimamizi wa kuleta mabadiliko.
Mafunzo hayo
yaliyofadhiliwa na Benki ya Dunia ni Utekelezaji wa Mpango Mkakati wa Miaka
mitano wa Mahakama ya Tanzania na yanalenga katika kuboresha utendaji kazi na
kuleta mabadiliko ndani ya Mahakama.
Kaimu Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe.
Prof. Ibrahim Juma (wa pili kushoto) akiwasili katika ukumbi wa AICC jijini
Arusha kuhudhuria Mafunzo ya Majaji yaliyoanza jijini humo.Kushoto kwake ni
Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Mhe. Ferdinand Wambali. Kushoto kwa
Jaji Wambali ni Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania Mhe. Katarina Revokati na
kulia ni Mkurugenzi Msaidizi wa Utawala wa Mahakama Bibi Wanyenda Kutta.
Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya
Tanzania Mhe. Ferdinand Wambali akifungua Mafunzo ya Majaji wa Mahakama Kuu ya
Tanzania katika Ukumbi wa AICC leo jijini Arusha. Mahakama inaendesha Mafunzo
kwa Majaji wote wa Tanzania ambapo Majaji wa Mahakama ya Rufani wanahudhuria
Mafunzo kuhusu namna ya kutoa maamuzi ya Mahakama katika usikilizwaji wa kesi
ngazi ya Rufaa, Majaji Wafawidhi kuhusu Usimamizi wa uendeshaji wa kesi wakati
Majaji wengine wanapatiwa mafunzo kuhusu uongozi na usimamizi wa kuleta
mabadiliko.
Waheshimuiwa Majaji wa Mahakama Kuu
ya Tanzania wakiwa kwenye ufunguzi wa Mafunzo yao yaliyoanza jijini Arusha.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...