Wadau wa malezi ya watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi (JSI) wametoa mafunzo ya mfumo jumuishi kwa watendaji na wakuu wa idara na vitengo wa Halmashauri ya Manispaa ya Temeke. 

Mfumo huo umewekwa na serikali kwa kushirikiana na wadau kama WAMATA na (JSI) ili kutoa huduma kwa pamoja kwa watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi pamoja na watu wanaoishi na virusi vya ukimwi na sio kila mdau kwenda au kupeleka huduma kipekee 

Akitoa mafunzo hayo Asia Jingu amesema mfumo huu ni muhimu kwani utawezesha kuweka taratibu za utoaji wa huduma kwa watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi na si kila taasisi ama mdau kuwa na utaratibu wake jambo ambalo lilikuwa likisababisha baadhi ya watoto kukosa huduma kutokana na sababu mbalimbali. 

Pia Mfumo huu utahamasisha ushirikiano wa karibu kati ya wadau na taasisi zinazojihusisha na kuhudumia watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi. 

Asia Jingu pia amesema watoa huduma kwa watoto wanaoishi katika mazingira magumu wanatakiwa kutoa huduma kwa uweledi mkubwa kwani kazi hii ni ya kujitolea,kwa hiyo kwa wale wote watakaopata mafunzo kwa ajili ya huduma hiyo katika Mitaa mbalimbali wawe waadilifu kwa watoto na pia kutoa huduma bila ubaguzi kwa watoto wala kutowadhuru watoto hao walio katika mazingira magumu.
Mkufunzi wa masuala ya malezi ya watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi (JSI), Asia Jingu akitoa mafunzo hayo kwa viongozi mbalimbali, watendaji na wakuu wa idara na vitengo wa Halmashauri ya Manispaa ya Temeke.


watendaji na wakuu wa idara na vitengo wa Halmashauri ya Manispaa ya Temeke wakiwa makini.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...