Kamishna
Jenerali wa Uhamiaji Nchini Dr. Anna Peter Makakala amefanya mabadiliko makubwa
ya Viongozi wa Uhamiaji wa Mikoa mbalimbali hapa nchini pamoja na kuwateua Wakuu
Wapya wa mikoa kushika nyadhifa hizo katika Mikoa iliyopo Tanzania Bara na Visiwani
Zanzibar.
Katika Mabadiliko haya Naibu Kamishna wa Uhamiaji Sixstus Faustine Nyaki
aliyekuwa Mkuu wa Uhamiaji Mkoa wa Mwanza amehamishiwa mkoa wa Simiyu wakati aliyekuwa Mkuu wa Uhamiaji Mkoa
wa Rukwa Naibu Kamishna wa Uhamiaji
Selemani Bandiho Kameya amehamishiwa Mkoa wa Tabora.
Mkuu wa Uhamiaji Mkoa wa Mbeya,
Naibu Kamishna wa Uhamiaji Asumsio
Paulus Achacha amehamishiwa Mkoa wa Kaskazini Pemba, Mkuu wa Uhamiaji
Mkoa wa Manyara Naibu Kamishna Peter Jerome Kundy amehamishiwa Mkoa wa
Dodoma kuchukua nafasi ya Kamishna
Msaidizi Ali Mohamed ambaye amehamishiwa kuwa Mkuu wa Uhamiaji mkoa wa Arusha.
Naibu
Kamishna wa Uhamiaji Mkemi Mhina Seif ameteuliwa kuwa Mkuu wa Uhamiaji Mkoa wa Kusini
Unguja, Naibu Kamishna wa Uhamiaji Muhsin
Abdallah Muhsin ameteuliwa kuwa Mkuu wa Uhamiaji Mkoa wa Kaskazini Unguja, Naibu Kamishna wa Uhamiaji Said Omary Hamdani ameteuliwa kuwa Mkuu wa Uhamiaji Mkoa wa Mjini Magharibi na Naibu Kamishna wa Uhamiaji Othman Khamis Salum ameteuliwa kuwa Mkuu wa Uhamiaji Mjini
Magharibi Unguja.
Katika
mabadiliko hayo baadhi ya Wakuu wa Uhamiaji wa Mikoa wamebaki katika Vituo vyao
vya kazi vya awali akiwemo aliyekuwa Mkuu wa Uhamiaji Mkoa wa Morogoro Naibu
Kamishna wa Uhamiaji Safina Muhindi, Mkuu
wa Uhamiaji Mkoa wa Lindi Naibu Kamishna wa Uhamiaji George Kombe, Mkuu wa
Uhamiaji Mkoa wa Ruvuma Naibu Kamishna
wa Uhamiaji Hilgaty Laurent Shauri, Mkuu
wa Uhamiaji Mkoa wa Singida Naibu Kamishna wa Uhamiaji Faith Alexander Ihano na Mkuu wa Uhamiaji Mkoa wa Mara Naibu Kamishna Fredrick Eustace Kiondo.
Wengine waliobaki kwenye vituo vyao vya awali
ni pamoja na Naibu Kamishna wa Uhamiaji Abdallah
Ramadhani Towo mkoa wa Kagera
na Naibu Kamishna wa Uhamiaji Anastazia
Gasper Ngatunga mkoa wa Shinyanga.
Katika
mabadiliko hayo Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dr. Makakala pia amewateua Viongozi wa Uhamiaji wa Mikoa wapya katika
baadhi ya mikoa hapa nchini ambapo Naibu Kamishna wa Uhamiaji Mary Francis
Palmer kuwa Mkuu wa Uhamiaji Mkoa wa Dar es
Salaam, Naibu Kamishna wa Uhamiaji Plasid
Mazengo, Mkuu wa Uhamiaji Mkoa
wa Pwani, Mrakibu Mwandamizi wa
Uhamiaji James Andrew Mwanjotile, Mkuu
wa Uhamiaji Mkoa wa Mtwara,
Kamishna Msaidizi Mwandamizi Hope
Jaffer Kawawa Mkuu wa Uhamiaji Mkoa wa Iringa, na Kamishna
Msaidizi wa Uhamiaji Hosea Alphonce
Kagimbo Mkoa wa Njombe.
Wengine
ni Naibu Kamishna wa Uhamiaji Rashid
Salum Magetta Mkuu wa Uhamiaji Mkoa wa Songwe, Naibu Kamishna wa Uhamiaji Carlos John Haule, Mkuu wa Uhamiaji Mkoa wa Rukwa, Naibu Kamishna wa Uhamiaji Julieth Deodatus Sagamiko Mkuu wa Uhamiaji Mkoa
wa Manyara, Naibu Kamishna wa Uhamiaji Albert Joseph Rwelamila, Mkuu wa
Uhamiaji Mkoa wa Kilimanjaro na Naibu Kamishna wa Uhamiaji Paul Laurent Eranga, Mkuu wa Uhamiaji Mkoa wa Mwanza.
Naibu
Kamishna wa Uhamiaji Crispin Crispin Ngonyani ameteuliwa kuwa Mkuu wa Uhamiaji
Mkoa wa Tanga, Naibu Kamishna wa Uhamiaji Shaban Omar Hatibu Mkuu wa Uhamiaji Mkoa wa Katavi,
Naibu Kamishna wa Uhamiaji Remigius
Ibrahimu Pesambili Mkuu wa Uhamiaji Mkoa wa Kigoma na Mrakibu Mwandamizi wa Uhamiaji
Novaita Edmund Mrosso ameteuliwa kuwa
Mkuu wa Uhamiaji Mkoa wa Mbeya.
Aidha
Mrakibu Mwandamizi wa Uhamiaji Bakari Mohamed Ameir ameteuliwa kuwa Mkuu wa Kituo
cha Uhamiaji cha Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume [AAKIA] na
Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhamiaji
Fulgence Andrew Mutarasha kuwa Mkuu wa Uhamiaji Kituo cha Uwanja wa Ndege wa
Kimataifa Julius Nyerere[JNIA].
Imetolewa na
Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Nchini
Dr. A. P. Makakala
3 Machi 2017
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...