Tarehe
23 May 1933 – 13 April 2007
Baba yetu mpendwa, Masaa, Siku, Wiki, Miezi
na sasa ni miaka 10 tangu Mungu wetu mwenye wingi wa rehema na upendo
alipodhihirisha utukufu na mapenzi yake makubwa kwako hadi akaamua kukuchukua
alfajiri ya siku ya Ijumaa terehe 13/04/2007.
Huzuni na majonzi bado vimebaki kuwa ni
sehemu ya maisha yetu katika familia lakini tunalo lile tumaini la Neno la
Mungu kuwa siku moja tutaufikia ule ufufuo wa milele ndani ya Kristo pamoja. Matendo
yako mema yamebaki kuwa lulu na mwanga uiangaziayo familia yetu. Maisha yako ya
upendo, unyenyekevu, uadilifu, utu wema na bidii katika kazi ndiyo dira
inayotuongoza: mke wako Mama Ahilai, watoto wako Sydney, Sarah, Oripa, Geoffrey,
Rodney, wakwe zako Pascal, Joel, Eunice na Salome pamoja na wajukuu zako
Dennis, Karen, David, Samantha, Jovin na Daniel. Tutakukumbuka siku zote kwa
kukukosa katika mengi.
Dada zako,
kaka zako na familia zao na ndugu wengine wote wa koo za Chiduo, Chitemo,
Chigongo, Mheta, na Msele nao pia wanakukumbuka sana. Kwetu sote imebaki
kumbukumbu ni jinsi gani ulikuwa mhimili wa familia na ukoo mzima kwa ujumla.
Baba,
kwako tulijifunza uaminifu, uadilifu, unyenyekevu na kupenda haki vitu ambayo
viliyokujengea heshima kubwa miongoni mwa jamii.
Mchango
wako mkubwa ulioutoa katika kulitumikia Taifa hili utakumbukwa siku zote na
wachapa kazi wote.
Bwana
alitoa na Bwana ametwaa. Jina la Bwana Lihimidiwe.
1 Wathesalonike 4:13-14 Neno: Bibilia Takatifu
13 Ndugu wapendwa, hatupendi mkose kujua kuhusu wale
wanaokufa, au mhuzunike kama watu wasiokuwa na tumaini. 14 Tunaamini kwamba
Yesu alikufa na kufufuka, kwa hiyo tunaamini kwamba Mungu atawainua wale
waliokufa pamoja na Kristo wakiwa ndani yake.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...