Tarehe 23 May 1933 – 13 April 2007

Baba yetu mpendwa, Masaa, Siku, Wiki, Miezi na sasa ni miaka 10 tangu Mungu wetu mwenye wingi wa rehema na upendo alipodhihirisha utukufu na mapenzi yake makubwa kwako hadi akaamua kukuchukua alfajiri ya siku ya Ijumaa terehe 13/04/2007. 

Huzuni na majonzi bado vimebaki kuwa ni sehemu ya maisha yetu katika familia lakini tunalo lile tumaini la Neno la Mungu kuwa siku moja tutaufikia ule ufufuo wa milele ndani ya Kristo pamoja. Matendo yako mema yamebaki kuwa lulu na mwanga uiangaziayo familia yetu. Maisha yako ya upendo, unyenyekevu, uadilifu, utu wema na bidii katika kazi ndiyo dira inayotuongoza: mke wako Mama Ahilai, watoto wako Sydney, Sarah, Oripa, Geoffrey, Rodney, wakwe zako Pascal, Joel, Eunice na Salome pamoja na wajukuu zako Dennis, Karen, David, Samantha, Jovin na Daniel. Tutakukumbuka siku zote kwa kukukosa katika mengi.

Dada zako, kaka zako na familia zao na ndugu wengine wote wa koo za Chiduo, Chitemo, Chigongo, Mheta, na Msele nao pia wanakukumbuka sana. Kwetu sote imebaki kumbukumbu ni jinsi gani ulikuwa mhimili wa familia na ukoo mzima kwa ujumla.

Baba, kwako tulijifunza uaminifu, uadilifu, unyenyekevu na kupenda haki vitu ambayo viliyokujengea heshima kubwa miongoni mwa jamii.
Mchango wako mkubwa ulioutoa katika kulitumikia Taifa hili utakumbukwa siku zote na wachapa kazi wote.

Bwana alitoa na Bwana ametwaa. Jina la Bwana Lihimidiwe.

1 Wathesalonike 4:13-14 Neno: Bibilia Takatifu


13 Ndugu wapendwa, hatupendi mkose kujua kuhusu wale wanaokufa, au mhuzunike kama watu wasiokuwa na tumaini. 14 Tunaamini kwamba Yesu alikufa na kufufuka, kwa hiyo tunaamini kwamba Mungu atawainua wale waliokufa pamoja na Kristo wakiwa ndani yake.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...