Tarehe 24 Novemba 2016 Wizara ilizindua Cheti kipya cha Chanjo
za Kimataifa kijulikanacho kama Cheti cha Chanjo ya Homa ya Manjano ili
kuendana na maboresho ya kipengele cha 7 cha Kanuni za Afya za Kimataifa za
mwaka 2005.
Lakini pia, zoezi hili lililenga kukabiliana na kusambaa kwa
vyeti vya kugushi (feki) ambavyo watu wamekuwa wakivipata bila kupata
chanjo, hali ambayo ilitishia Afya ya Jamii dhidi ya ugonjwa huo. Kwasababu
hizo, Wizara iliona ni vema kufanya mabadiliko ya cheti hicho, ambapo wenye
vyeti vya zamani wanabadilishiwa na wale wanaopata chanjo wanapewa cheti
kipya.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...