Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotion Bw. Alex Msama akizungumza na waandishi wa habari leo ofisini kwake Kinondoni,jijini Dar es salaam kuhusiana na maandalizi ya tamasha la Pasaka linalotarajiwa kufanyika Aprili 16 kwenye uwanja wa Uhuru na kutumbuizwa na waimbaji wa muziki wa injili kutoka mataifa mbalimbali na nchini Tanzania.
Msama amesema mwimbaji nguli kutoka nchini Afrika ya Kusini Solly Mahlangu atakuwa ni mmojawapo wa waimbaji kutoka nje ya nchi wakiwemo wengine kutoka nchini Kenya, Ameongeza kuwa tamasha hilo litafanyika pia katika mikoa ya Mwanza na Simiyu, hata hivyo tamasha hilo halitafanyika katika mkoa wa Dodoma kama ilivyotangazwa awali kutokana na uwanja wa Jamhuri ambao ulikuwa utumike siku hiyo kuwa na shughuli nyingeni.
Msama
amesema kuwa katika tamasha hilo la Pasaka litakalofanyika katika
Uwanja wa Uhuru,Mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Waziri wa Mambo ya
Ndani,Mh.Mwigulu Nchemba,baada ya tamasha hilo kurindima jijini Dar
litahamia Simiyu na jijini Mwanza ambako mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Angeline Mabula .
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...