Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Tanga
Mhe. Imani Abood Muonekano wa majengo ya Mahakama Kuu
kanda ya Tanga baada ya kukamilika kwa ukarabati
Na Lydia Churi- Mahakama

Mahakama ya Tanzania kupitia Mpango Mkakati wake wa miaka mitano (2015/16-2019/2020) pamoja na Mradi wa Maboresho ya huduma za Mahakama, imepania kuhakikisha kuwa kesi zote za zamani pamoja na zile zinazosajiliwa zinamalizika ili wananchi waweze kuwa na kujenga imani zaidi na chombo hicho muhimu cha utoaji wa haki nchini. Katika kulitekeleza hili, ipo mikakati iliyowekwa na Mahakama kwa ujumla na ile inayowekwa na kila Kanda ya Mahakama Kuu nchini.

Mikakati ya Mahakama ni pamoja na Majaji na Mahakimu kupangiwa idadi ya kesi watakazotakiwa kuzisikiliza na kuzimaliza katika kipindi cha mwaka mmoja. Kila Jaji amepangiwa kumaliza kesi 220 kwa mwaka na kila hakimu anatakiwa kusikiliza kesi 250 kwa mwaka. Mkakati mwingine wa jumla ni kiwango cha muda kilichopangwa kwa kesi kukaa Mahakamani, mathalani, Mahakama ya Tanzania imepanga kuwa kesi zote zilizosajiliwa Mahakama Kuu zisikae Mahakama kwa muda unaozidi miaka miwili wakati katika Mahakama za Hakimu Mkazi pamoja na zile za wilaya imeamuliwa kesi isizidi miezi 12 Mahakamani. Kesi katika Mahakama za Mwanzo inatakiwa kumalizika katika kipindi cha miezi sita.

Aidha, Mahakama imeanzisha utaratibu wa kufanya vikao na wadau wake ili kujadili namna ya kumaliza kesi kwa wakati kama moja ya mikakati yake ya kuhakikisha kesi zote za zamani zinamalizika Mahakama na pia kesi zinazosajiliwa zinamalizika kwa wakati ili kutimiza wajibu wake wa kikatiba wa kuwapatia wananchi wa Tanzania Haki sawa na kwa wakati.

Pamoja na kuwepo kwa mikakati ya Mahakama ya kumaliza kesi zilizoko Mahakamani, Mahakama Kuu kanda ya Tanga nayo imejiwekea mikakati yake ili kuhakikisha inaenda sambamba na kasi ya Mhimili huo ya  kuhakikisha wananchi wanapata haki kwa wakati kwa kumaliza kesi zao kwa wakati.

Akizungumzia suala la kumalizika kwa kesi kwa wakati, Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu kanda ya Tanga Mheshimiwa Imani Abood alisema kanda yake imepanga kuwanunulia Mahakimu wake wote (68) kompyuta Mpakato (Laptops) zitakazowasaidia katika kurahisisha kazi zao na kuondosha mashauri kwa wakati katika Mahakama mbambali za mkoa wa Tanga. Alisema lengo ni kuhakikisha Mlundikano wa kesi zilizopo Mahakamani unaisha na pia kesi zinazosajiliwa zinamalizika kwa wakati.

Jaji Mfawidhi alifafanua kuwa kompyuta hizo zitawasaidia waheshimiwa Mahakimu katika kuandika hukumu ili wananchi waweze kupati haki kwa wakati. Aliongeza kuwa hivi sasa Mahakimu wa mahakama za Mwanzo huandika hukumu kwa kalamu na baadaye hukumu hizo hupelekwa kwenye mahakama za wilaya ambapo kuna umeme kwa ajili ya kuchapwa na baadaye hurudishwa kwenye kwenye Mahakama za Mwanzo.

Alisema pia kanda yake inakabiliwa na uhaba wa watumishi hasa Makatibu Muhtasi pamoja na vitendea kazi jambo ambalo limekuwa likichelewesha utolewaji wa hukumu pamoja na upatikanaji wa nakala za hukumu kwa wakati. Aliongeza kuwa kwa Mahakimu kupatiwa kompyuta hizo kutarahisisha upatikanaji wa haki.
Pamoja na kuwapatia Mahakimu Kompyuta, Jaji Abood alisema Mahakama Kuu Kanda ya Tanga inao mpango wa kuhakikisha inazipatia umeme baadhi ya Mahakama za Mwanzo kupitia Mradi wa Umeme vijijini (REA) ili kurahisisha upatikanaji wa nakala za hukumu kwa wakati. Na hivi sasa tayari Mahakama za Mwanzo tano zimeshapatiwa umeme.

BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...