Na Judith Mhina-MAELEZO

Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ulikuja hapa duniani Aprili 13, 1922 kupitia kwa Mpendwa Marehemu Bibi Mgaya wa Buritho kama zawadi kwa nchi ya Tanzania.

Mwalimu tunamshukuru Mungu kwa kutupa wewe ambaye umeitendea mambo makubwa Tanzania, Afrika na Dunia kwa ujumla.

Mwalimu wakati nakumbuka kuzaliwa kwako nimepata fursa ya kuangalia kazi ulizozifanya mara baada ya kuacha madaraka ya Urais na kujikita katika kazi kuu tano; Mosi pamoja na kubaki na kofia moja ya Uenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), ya kuimarisha Chama na alianza maandalizi ya kukabidhi Uenyekiti huo kwa Rais aliyepokea madaraka ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye alikuwa Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Mzee Ali Hassan Mwinyi.

Pili, mwaka 1986 baadhi ya Viongozi wa nchi za Kusini mwa Dunia, walikuomba kuanzisha Tume ya Uchambuzi wa maendeleo ya nchi za Kusini tangu miaka 30 iliyopita na kuweza kuona hatua za maendeleo na changamoto zilizopo katika mataifa hayo na mapendekezo ya nini kifanyike ili kuboresha ustawi wa wananchi.

Mwalimu Nyerere alikubali jukumu hilo, ndipo alianza kutembelea nchi 19 katika Bara la Asia na Marekani ya Kusini kwa ajili ya kuanza utekelezaji wa majukumu hayo mapya. Safari ya kutafuta maoni hayo ilikuwa ni pamoja na kupata uthibitisho wa kuwaelewesha wananchi na nchi hizo kuhusu majukumu ya Tume na aina ya maoni yanayokusanywa.

Kazi hiyo aliifanya kwa miaka mitatu na kutoa ripoti kuwa nchi za Kusini zifanye maendeleo yao yenyewe yalenge maslahi ya wananchi walio wengi kwa kielelezo kuwa ili nchi za Afrika ziweze kupiga hatua za maendeleo ni vyema ziwe na mshikamano kama zinahitaji kushindana na nchi za Kaskazini.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...