Na  Bashir  Yakub.

Yapo  mambo  unayotakiwa  kufanya  mara  tu  baada  ya  kusajili  kampuni.  Tunazungumzia  yale  utakayoyafanya ule  mda  baada  ya  kuwa   umepewa    cheti  cha  kuzaliwa  kwa  kampuni( certificate  of  incorporation)  kutoka  BRELA.  Mambo  haya  ni  ya  kisheria  na  kutoyafanya  kwake  kunahesabika  ni  kuvunja  sheria.  Kwahiyo  mambo  haya ni  lazima  na  sio  hiari. 

Hata  hivyo  kabla  ya  kueleza hayo  ni  muhimu  tukajikumbusha kuhusu  taratibu  za  kusajili  kampuni.  Tunasema  kujikumbusha  kwakuwa makala  kuhusu  taratibu  na  namna  ya  kusajili/kuunda  kampuni   hatua  kwa  hatua   yalishaandikwa  hapo  awali.  Haya  yote  yatakuwa  yakitoka   Sheria  ya  Makampuni ,Namba 12  ya  mwaka  2002.

1.HATUA  ZA  KUSAJILI/KUUNDA  KAMPUNI.          
( a ) Kwanza  hakikisha  unajua  unahitaji  kufanya  biashara  gani.  Hii  ni  kwasababu  katika  vitabu  vya  kampuni  lazima  uandike  biashara  unayotaka  kufanya  au  unayofanya   tayari.

( b ) Hakikisha  mko  wawili  au  zaidi.  Hakuna  kampuni  ya  mtu  mmoja. Kampuni  binafsi  huanzia  watu  wawili  na mwisho  ni  watu  50. Unaweza kuwa  wewe na  mke  wako,  rafiki,  ndugu,  mzazi, mtoto  nk.

( c ) Fahamu  kampuni  yenu  inatakiwa kuwa  na  hisa  ngapi  na  kila  hisa  itakuwa  inauzwa  bei  gani. Pia  unatakiwa  kujua  kampuni  itakuwa  na  mtaji  wa  shilingi  ngapi.   Kwa mfano  kampuni  itakuwa  na  hisa  10000,  bei  ya kila  hisa  ni  Tshs 1000 ambapo,  hisa x bei  ya  hisa = mtaji  wa  kampuni, kwa  maana  ya  10000 x 1000 =  10000000 ambao  ndio  mtaji  wa  kampuni.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...