Na  Bashir  Yakub
Ni  kipindi  muhimu  kujua  kuhusu  hisa. Hivi  karibuni  utakuwa  umesikia  makampuni  mbalimbali  hasa  yale  ya  simu  yakiwatangazia  watu  kununua  hisa.  Ni muhimu  kwako  kujua  kuhusu  biashara  hii.  Huenda  ikawa  ya  faida  kwako   au eneo  zuri   kwako  kwa  kuwekeza.
Mapema  niseme  kuwa  usiogope wala usiwe  mwenye  hofu. Biashara  ya  hisa  ni  ya  watu  wote tajiri  au  maskini.  Laki  moja,  laki mbili  nk.  unaweza  kununua  hisa.  Ili umiliki  hisa kwenye kampuni  ya  simu  si  lazima  umiliki  mamilioni  kama  unavyodhani.  Na  hapa  ndipo  tunapokosea na  kuwaacha  matajiri  watambe  nasi  tubaki  kulalamika.

1.HISA  NI NINI.
Hisa  ni  mali  kama  zilivyo  mali  nyingine  unazomiliki. Tofauti  ya  hisa  na mali  nyingine ulizonazo  kama  shamba,  gari,  nyumba  nk.ni  kuwa    mali   nyingine  huweza  kushikika   au  kuonekana  kwa  macho  wakati  hisa  ni  mali  isiyoonekana  kwa  macho.  Yumkini  zote  ni  mali  tu.
Hisa  ni  maslahi  au  haki  fulani  unayokuwa nayo  katika  taasisi au  kampuni  fulani.  Ndiyo  maana  ni  mali  isiyoonekana  kwasababu  huwezi  kuona  maslahi  au  haki  kwa macho.

2.  KUMILIKI  HISA  KATIKA  KAMPUNI.
Kampuni  yoyote  unayoiona huwa  inao  wanahisa.  Wanahisa  ndio  wamiliki  wa  kampuni.  Kwahiyo  hata  wewe  ukinunua  hisa  kwenye  kampuni  yoyote  na  wewe  unakuwa  mmoja  wa wamiliki. 
Haijalishi  ukubwa  wa kampuni  na  kiwango  chako cha  hisa ulichonunua  bali  ni  kuwa  ukishanunua  tu   hapohapo  na  wewe  unakuwa  mmoja  wa  wamiliki. Hata  hisa  za  laki  moja  nazo  zinakufanya kuwa  mmoja  wa  wamiliki.
Kiwango cha  hisa  zako  ndicho  kiwango  cha  umiliki  wako.  Kampuni  ikiwa  na  hisa  100,000   na  wewe  ukamiliki  hisa 50,000  basi  wewe  unaimiliki  nusu  ya  kampuni.  Ukimiliki  hisa  25,000  basi  wewe  unamiliki  robo  ya  kampuni.  Halikadhalika  ukimiliki  hisa  500,  100,  50,  10, 5  au  hata  hisa  3  basi  hichohicho  kiwango  chako  cha  hisa  ulichonunua   ndicho  kiwango  chako cha  umiliki   wa  kampuni  husika. 
Kwahiyo  ukinunua  hisa  100  Vodacom  basi  wewe  utaimiliki  Vodacom  kwa  kiwango  cha hisa hizo  ulizonunua. Isipokuwa  ni  muhimu  kujua  kuwa  anayemiliki  hisa nyingi  kuliko  wote  ndiye  hujulikana  kama  mmiliki  mkuu  wa  kampuni.

3.  JE  UTAFAIDIKAJE  NA  HISA.
Kila  mwanahisa  hupata  gawio  la  faida  pale  kampuni  inapotangaza  faida.  Kampuni  hutangaza  faida  kila  baada  ya  mwaka  au  nusu  mwaka  au  vinginevyo.

 Utapata  mgao  kwa  asilimia  kutokana  na  kiwango  chako  cha  hisa  ulizonazo. Ukiwa  na  hisa  nyingi  utapata mgao  mkubwa,  ukiwa  na  hisa  kidogo  utapata  mgao  mdogo   na  vivyo  hivyo. 

Kusoma zaidi BOFYA HAPA



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...