Kwenye
muungano huo ambao unaitwa Taifa Moja, makampuni matatu makubwa ya
kutoa huduma za simu za mkononi ya Tigo Tanzania, Airtel Tanzania na
Zantel, wateja wanaweza kutuma pesa na kupokea kutoka kwenye moja ya
mitandao hiyo kwa gharama zile zile.
Hapo
awali, kutuma pesa au kupokea pesa kutoka mtandao tofauti mteja alikuwa
akipokea ujumbe mfupi ambao ilikuwa ni lazima apeleke kwa wakala wa
mtandao ambao amepokea fedha kutoka na ilikuwa izizidi siku saba tofauti
na hapo fedha hiyo ilikuwa inarudi kwa aliyetuma.
Kwa
huduma hii, mteja anapaswa kuchangia huduma ya kutuma pesa kutoka kwa
menu ya kawaida, halafu anachangua kutuma pesa kwenda mitando mingine.
Akizungumza
jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki wakati wa kutembelea watumiaji
wa huduma za kutuma na kupokea pesa, Meneja wa Airtel Money kutoka
kampuni ya Airtel Tanzania Moses Alphonce alisema kupitia muungano wa
Taifa Moja wameweza kuwafanya wateja wapate njia rahisi ya kutuma na
kupokea fedha.
Tunajua
hapo zamani kuna baadhi ya wateja walikuwa wanapata wakati mgumu
linapokuja suala la kutuma na kupokea fedha. Ilikuwa aidha upokee fedha
kwa ujumbe mfupi au uwe na laini ya simu zaidi ya moja. Ukipokea fedha
kwa ujumbe na kwa bahati mbaya ukaufuta ilikuwa inamaanisha fedha
imepotea, alisema Alphonce.
Meneja wa Airtel Money kutoka kampuni ya Airtel Tanzania Moses Alphonce akitoa elimu kwa mmoja wa watumiaji wamitandano ya simu kwa namna Makampuni ya simu za mikononi nchini yameungana kwa kutoa huduma za kutuma na kupokea fedha kwenda mitandao yeyeto nchini kwa kiwango cha gharama ile ile.
Makampuni ya simu za mikononi nchini yameungana kwa kutoa huduma za kutuma na kupokea fedha kwenda mitandao yoyote nchini kwa kiwango cha gharama ile ile.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...