Basi la abiria linalofanya safari zake kati ya Makumbusho mpaka Posta, limepiga mweleka na kuingia mtaroni katika eneo la Oysterbay, Kinondoni jijini Dar es salaam mchana wa leo.

imeelezwa kwamba Basi hilo lenye namba za usajili T 958 DEJ aina ya Hino lililokuwa likitokea Posta kuelekea upande wa Moroco, lilijikuta likiingia mtaroni humo, baada ya dereva wake kushindwa mbinu za kulizuia kufuatia gari nyingine iliyoingia ghafla barabarani ikitokea upande wa Kituo cha Polisi Oysterbay, hivyo kutokana mwendo kasi wa basi hilo, ilishindwa kusimama na kuparamia mti uliokuwa kando ya barabara na kuingia mtaroni.

Inadaiwa kuwa abiria wote waliokuwepo kwenye basi hilo walitoka salama na kuendelea na safari zao.
Hivi ndivyo muonekano wa Basi hilo baada ya kuparamia mti.
Mashuhuda wa Ajali hiyo wakiwa katika eneo la tukio.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Hahahahahah dereva aliingia ktk gari ya polisi nilidhani ambulance shida kweli. Ntarudi baada 50.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...