ZAIDI ya miradi 25 inatarajiwa kutekelezwa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii Nchini kama sehemu ya kushiriki katika ujenzi wa Uchumi wa viwanda Nchini.

Hayo yalisemwa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii Nchini, Meshach Bandawe (pichani) wakati alipokuwa akiwasilisha mada ya ushiriki wa Mifuko ya Hifadhi katika Ujenzi wa uchumi wa Viwanda katika mkutano wa wanachama na wadau wa Mfuko wa PPF uliofanyika Jijini Arusha hivi karibuni.

Bandawe alisema kuwa Miradi hiyo itahusu viwanda vitakavyotekelezwa na Mfuko mmoja mmoja pamoja na Viwanda vitakavyotekelezwa na Mifuko yote kwa pamoja kupitia Umoja wao wa TSSA (Tanzania Social Security Association). 

"Viwanda hivyo ambavyo vipo katika hatua mbalimbali za utekelezaji, inajumuisha baadhi ambavyo vimeanza uzalishaji na vingine vipo katika hatua za kufanyiwa upembuzi yakinifu ambavyo kati ya hivyo vipo ambavyo vilisimama uzalishaji ambavyo vitahitaji kufufuliwa, vipo ambavyo vilikuwa vikisuasua katika uzalishaji na uendeshaji ambavyo vitahitaji kuendelezwa na vingine vitajengwa upya". alisema Bandawe.
Alivitaja Baadhi ya Viwanda hivyo kuwa ni Kiwanda cha Sukari cha Mkulazi na Mbigili, viatu Karange Moshi, Vinu vya NMC Iringa, Dodoma na Mwanza, Viuadudu Kibaha, General Tyre Arusha, Chai Mponde, Nguru Ranch Morogoro, Mvinyo na Juisi ya Zabibu Dodoma, Kilimanjaro Machine tools, Tandahimba na Newala Cashewnut Union, sukari ya sweetner Tanga, Kilimo cha Wanga Lindi, Kiwanda cha Madawa TPI, Chai Kagera, Morogoro Canvas, Urafiki Dar es Salaam, Vunu vya kuchambulia pamba vya Nyanza Cooperative Union, Viwanda vya Ngozi na bidhaa za Ngozi, Maji tiba na Bidhaa za pamba za Hospitali Mkoani Simiyu na Shinyanga nk.

Viwanda hivi ambavyo vina mnyororo mrefu wa uogezaji thamani vitategemea mali ghafi kutoka ndani ya Nchi, vitahusu pia bidhaa zinazotumiwa na watu wengi kwa ajili ya soko la ndani na Nje ya Nchi, vitatengeneza ajira nyingi na hivyo pia kupanua wigo wa wanachama wengi watakaojiunga na Mifuko hiyo na baadae kuimarisha uchumi wa Nchi.

Uwekezaji huu wa viwanda utakuwa wenye tija kwa wanachama, mifuko na taarifa kwa ujumla na miradi yote itafanyiwa upembuzi yakinifu ili kuhakikisha usalama wa fedha za wanachama na itafuata kanuni taratibu na miongozo mbalimbali ya uwekezaji na wataalam watatumika katika hatua mbalimbali za utekelezaji. Viwanda hivi vitakapokamilika vinategemewa kuzalisha ajira zaidi ya watu 114,000 Nchini.

Umoja a Mifuko ya Hifadhi unaundwa na Mifuko ya NSSF, PPF, LAPF, PSPF, GEPF, NHIF, WCF na ZSSF uliopo Zanzibar.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Waheshimiwa msisahau core business yenu maana naona mko vere bize na viwanda huku mnasahau kuandikisha, kulipa mafao na kuboresha huduma zenu. Najua mtasema mnafanya yote kwa pamoja ila si vibaya tukiwakumbusha. Na hizo ajira 114000 mnazozungumzia ni kwa raia au Magereza na JKT? Kuhusu General Tyre msomeni Sameer Africa na kuhusu sukari fuatilieni kwa karibu ugumu wa uzalishaji/ ushindani unaovikumba viwanda vya sukari Kenya. Si vibaya pia mkikaribisha private investment ili kugawana risks.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...