Muhadhiri wa chuo kikuu cha Afya na Tiba Muhimbili,Profesa Projestine Muganyizi akifafanua jambo mbele ya wadau na watafiti mbalimbali wa Afya,alipokuwa akitoa mrejesho wa utafiti walioufanya mkoani Njombe,uliohusu Afya ya Mama na Mtoto,jijini Dar.

Prof.Muganyizi alisema kuwa walikwenda Mkoani Njombe na kukutana na Wafanyakazi na viongozi wa Afya mkoani humo,mwaka jana mwezi wa sita na kufanya utafiti katika suala zima la Afya ya Mama na Mtoto.

Katika utafiti huo,anaema walibaini mambo makuu manne,kwanza 
ilikuwa suala la usafi katika hospitali zenyewe,kwa mazinginra ya nje vituo vingi vilikuwa vikionekana ni visafi,lakini kwa ndani ilibainika kuwa na mapungufu makubwa hasa katika eneo la usafi,Pili ni Katika uelewa wa kutoa huduma ya Afya,huduma za Mama na Mtoto zilikuwa na Mapungufu,wafanyakazi wengi walikuwa hawana weledi wa kutosha,

Anasema na kuongeza kuwa eneo la tatu ni katika suala la ufautiliaji wa hali ya Mama akiwa Mja mzito,vituo vingi havikuwa na uelewa wa kutumia hizo kadi ,akina Mama wengi walikuwa hawafuatiliwa kwa ukaribu wakiwa na uchungu, Mwisho ni suala la kuweka Kumbukumbu za Mama akiwa kwenye uchungu,ikabainika vituo vingi hazitumii zile kumbu kumbu na jambo lingine ni suala la Huduma inayotolewa kwa Mama Mzazi,Je meridhika vipi huduma aliyopewa kutoka kwa wale wahudumu wa afya,Iakabainika kuwa akina Mama wengi walikiri wazi kuwa walihudumiwa vizuri.

Shirika la Umoja wa Mataifa linalowahudumia watoto (UNICEF) lilipokea mrejesho huo,na kwa kuwa Shirika hilo lilikuwa likisaidia kuendeleza huduma ya Afya ya Mama na Mtoto,tayari limeanza kuzifanyia kazi changamoto zote zilizo ainishwa kwenye utafiti huo,ikiwemo na kuwaelemisha wahusika wote katika suala zima la Afya la kupunguza vifo vya mama na Mtoto.
Baadhi ya wadau na Watafiti wa Afya wakifuatilia mrejesho wa utafiti uliofanywa mkoani Njombe,uliohusu Afya ya Mama na Mtoto.
Mmoja wa Wakilishi kutoka UNICEF,akichangia mrejesho wa utafiti huo uliofanywa mkoani Njombe Mwaka jana, UNICEF wamekuwa wakishiriki kwa kiasi kikubwa katika kusaidia kuendeleza huduma ya Afya ya Mama na Mtoto mkoani Njombe.
Mhadhiri wa chuo kikuu cha Afya na Tiba Muhimbili,Profesa Projestine Muganyizi akichangia jambo mbele ya wadau na watafiti mbalimbali wa Afya,mara baada ya kutoa mrejesho wa utafiti walioufanya mkoani Njombe,uliohusu Afya ya Mama na Mtoto,jijini Dar.
Mkurugenzi wa kuratibu na kutunza utafiti kutoka Taasisi ya utafiti wa magonjwa ya binadamu nchini Tanzania (NIMR),Dkt Julius Massanja akitoa ufafanuzi wakati wa kusikiliza Mresho wa Utafiti uliofanyika Mkoani Njombe uliohusu Afya ya Mama na Mtoto.Dkt Massanja alisema kuwa katika utafiti huo .kazi ya mwanzo ilikuwa ni kujua na kubaini tatizo gani,hivyo Kufuatia mrejesho wa utafiti huo wa Afya ya Mama na Mtoto uliofanywa Mkoani Njombe,Shirika la UNICEF limeanza kurekebisha mambo mbalimbali yaliyobainishwa katika tafiti hiyo ikiwemo na kuwaelemisha wahusika wote katika suala zima la Afya la kupunguza vifo vya mama na Mtoto. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...