Msanii
wa bongo Fleva kutoka Tanzania Ibrahim Musa aka Roma Mkatoliki
akizungumza na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa Idara ya Habari
Maelezo jioni hii wakati akizungumzia sakata la kutekwa kwake pamoja na
wasanii wenzake katika studio ya Tongwe Records iliyopo Masaki jijini
Dar es salaam, Roma ameiomba serikali kuwahakikishia ulinzi wasanii
pamoja na watanzania kwa ujumla kwakuwa inaonesha hawana usalama kabisa
kutokana na tukio lenyewe lilivyowatokea , kushoto ni Waziri wa habari ,
Utamaduni Sanaa na Michezo Dk. Harisson Mwakyembe.
Roma Mkatoliki akifafanua zaidi kwa waandishi wa Habari kwa namna alivyotendewa na hao waliowateka.
Roma akiwaonesha wana habari namna alivyojeruhiwa na waliokuwa akiteswa na
hao watekaji ambao mpaka sasa hawajajulikana ni akina nani,kufuatia
Uchunguzi/upepelezi wa tukio hilo ukiendelea.
Waziri wa habari , Utamaduni Sanaa na Michezo Dk. Harisson Mwakyembe
akimsikiliza kulia Msanii wa bongo Fleva kutoka Tanzania Ibrahim Musa
aka Roma Mkatoliki akizungumza na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa
Idara ya Habari Maelezo jioni hii wakati akizungumzia sakata la kutekwa
kwake paoja na wasanii wenzake katika studio ya Tongwe iliyopo Masaki
jijini Dar es salaam, Roma ameiomba serikali kuwahakikishia ulinzi
wasanii pamoja na watanzania kwa ujula kwakuwa inaoyesha hawana usalama
kabisa kutokana na tukio lenyewe lilivyowatokea , kushoto ni Mkewa wa
Msanii huyo Bi Nancy.
PICHA NA MICHUZI JR
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...