Mwili wa Mbunge wa Viti Maalumu (CHADEMA) Hayati Dkt. Elly Macha unatarajiwa kuwasili nchini Aprili 20 mwaka huu ukitokea nchini Uingereza.
Dk Macha alifariki dunia Machi 31 mwaka huu katika Hospitali ya New Cross, Wolverhampton nchini Uingereza alikokuwa akitibiwa.
Akitoa ratiba ya msiba huo leo bungeni, Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai alisema taratibu zote za nchi i Uingereza za kurudisha mwili wa Mbunge huo zimekamilika.
“Kule kuna taratibu nyingi za kisheria na kadhalika haikuwa rahisi kuharakisha mchakato huo. Tunashukuru ubalozi wetu wa nchini humo umeweza kufanikisha jambo hili,”amesema
Ndugai amesema mwili wake utawasili Alhamis ya wiki ijayo katika uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere April 20, mwaka huu saa tisa mchana.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...