Mbunge wa Jimbo la Kishapu mkoani Shinyanga, Suleiman Nchambi amewataka wananchi kuwa kichocheo cha miradi ya maendeleo katika maeneo yao bila kujali msingi ya tofauti zao.

Nchambi alisema hayo jana wakati akiongoza kikao cha Kamati ya Mfuko wa Jimbo kilichofanyika katika Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu ambapo jumla y ash. Milioni 82 zinatarajiwa kutolewa kwa ajili ya shughuli za maendeleo.

Katika kikao hicho kilichohudhuria pia na madiwani, watendaji mbalimbali na viongozi wa dini alisema wananchi wanaoibua miradi ya maendeleo na Serikali kupitia Mfuko wa Jimbo inawapelekea fedha ili zitumike kufanya miradi hiyo.

Alisema viongozi wa ngazi za kata wakiwemo madiwani na watendaji wana nafasi ya kuhamasisha wanancho wao kushiriki katika shughuli za maendeleo na kutoa elimu kuhusu fedha za mfuko huo.Mbunge huyo alibainisha kuwa katika mwaka huu fedha zinazotarajiwa kutolewa katika jimbo hilo zitasaidia katika kukamilisha miradi mbalimbali ya maendeleo katika kata mbalimbali. 
Mbunge wa Jimbo la Kishapu mkoani Shinyanga, Suleiman Nchambi akifungua kikao cha Kamati ya Mfuko wa Jimbo kilichofanyika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya Kishapu.
A 1
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu, Stephen Magoiga akisisitiza jambo wakati akizungumza wakati hicho kikao hicho.
A 2
Wajumbe wa Kamati ya Mfuko wa Jimbo kutoka kushoto, Grace Chamila, Mh. Regina, Salma Kalebo na Thomas Ng’ombe wakifuatilia kikao hicho.
A 5
Mbunge wa zamani wa Jimbo la Kishapu ambaye ni Diwani wa Kata ya Uchungani wilayani humo, Paul Makolo akitoa uzoefu wake kuhusu namna ya fedha za Mfuko wa Jimbo zinavyofanya kazi wakati wa kikao hicho.
A
Washiriki wa kikaao hicho wakiwemo madiwani, watendaji kata, vijiji, wenyeviti wa vijiji, maafisa tarafa na viongozi wakifuatilia kikao hicho.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...