Mfuko wa Pensheni wa PPF unashiriki katika Maonesho ya Mifuko ya uwezeshaji Wananchi kiuchumi kwa ajili ya kutoa elimu juu ya Mafao yanayotewa na Mfuko huo.

PPF inatoa Mafao mbalimbali na katika Maonesho haya unatoa elimu juu ya mfumo wa ' Wote scheme' kwa sekta isiyo rasmi yaani wale wanaojiajiri kama vile mama lishe, dereva boda boda, wakulima, wafugaji, wajasiriamali, Wasanii, wote hawa wanathaminiwa na PPF ndio maana unato fursa za huduma za afya, mikopo ya maendeleo, mikopo ya Elimu na Mafao ya uzeeni.

Kupitia Maonesho haya PPF inasajili wanachama wapya hapo hapo viwanjani pamoja na kukabidhi vitambulisho vya uanachama wa Wote scheme.Hivyo ni fursa muhimu kwa wakazi wa Dodoma kufika katika viwanja vya Maahujaa kupata elimu hii muhimu na kujiunga na Mfuko huu ili kufaidika na Wote scheme.

Na kwa wale ambao hawapo Dodoma, wanaweza kutembelea Ofisi za PPF zilizopo karibu nao 
Waziri mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa akimpongeza mmoja wa wafanyabiashara wa kilimo cha pamba Riyaz Haider wakati wa akitembelea maonesho ya mifuko ya uwezeshaji wananchi Kiuchumi, baada ya mfanyabiashara huyo kupata mkopo kutoka katika benki kuu ya Tanzania kupitia benki ya NMB.
Mkurugenzi mtendaji wa asasi inayochochea uwekezaji sekta binafsi kwenye kilimo ( PASS ) Nicomedy Bohai akimuelezea mafanikio ya asasi hiyo Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa wakati wa maonesho ya mifuko ya uwezeshaji Wananchi Kiuchumi yanayofanyika katika viwanja vya mashujaa mkoani Dodoma. 
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa akitoa cheti kwa Mfuko wa Pensheni wa PPF kwa udhamini wa Maonesho ya Mifuko ya uwezeshaji Wananchi kiuchumi kwa Meneja wa PPF Kanda ya Mashariki na Kati Michael Christian ambaye alimwakilisha Mkurugenzi Mkuu wa PPF William Erio, kushoto ni Waziri wa Nchi ofisi ya Waziri Mkuu, Sera ,Bunge, Vijana, Ajira na watu wenye ulemavu Mhe.Jenista Mhagama. 
Mzee Seleman Saleh akiwasikiliza Linda Mshana meneja wa mikopo kushoto na Mary Kapeja mkuu wa kitengo cha masoko na biashara wa UTT Microfince PLC kulia katika maonesho ya mifuko ya uwezeshaji Wananchi kiuchumi. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...