Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe (katikati) akizungumza wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa 24 wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo uliofanyika leo terehe 10 Aprili, 2017 katika ukumbi wa LAPF mjini Dodoma. Kushoto ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt. Aloyce Nzuki na Mwenyekiti wa Baraza hilo, Esther Malima. 
NA HAMZA TEMBA - WMU

Waziri wa Maliasili na Utalii Prof. Jumanne Maghembe ametangaza mabadiliko makubwa katika biashara ya mkaa nchini na kusema kuwa kuanzia mwezi Julai mwaka huu hakuna mkaa wowote utakaosafirishwa kutoka wilaya moja kwenda nyingine ili kunusuru misitu inayoteketea kwa kasi hapa nchini.

Amesema hayo leo wakati akifungua mkutano wa 24 wa baraza la wafanyakazi wa Wizara ya Maliasili na Utalii uliofanyika katika ukumbi wa LAPF mjini Dodoma na kuhudhuriwa na wajumbe mbalimbali kutoka kwenye Idara, Vitengo na Taasisi mbalimbali zilizopo chini ya Wizara hiyo.

“Kuanzia mwezi Julai hakuna ruhusa ya kutoa vibali vya kuhamisha mkaa kutoka wilaya moja kwenda wilaya nyingine, mkaa utachomwa, utauzwa ndani ya wilaya kwa ajili ya matumizi ya watanzania wanaohitaji nishati ya mkaa, lakini biashara ya mkaa ya kutoa Dodoma kwenda Dar es Salaam mpaka Zanzibar marufuku.

Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe (kulia) akizungumza wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa 24 wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo uliofanyika leo terehe 10 Aprili, 2017 katika ukumbi wa LAPF mjini Dodoma.

“Wamekata misitu yetu yote, mito yetu imekauka, tunashindwa kupata maji ya umwagiliaji kwasababu watu wengi huko nje wanataka mkaa wetu, Tanzania jamani sio shamba la bibi, wale wote watakaotoa mkaa kutoka eneo moja hadi jingine kinyume na sheria hii watashuulikiwa kwa utaratibu wa uhujumu uchumi”, amesema Maghembe.

Amesema kuwa kwa upande wa miji mikubwa kama Dar es Salaam, Dodoma, Morogoro na Tanga vitaanzishwa viwanda maalumu vya kuzalisha mkaa ambao utauzwa kwa vibali maalumu katika mikoa mbalimbali hapa nchini. Amesema mkaa huo hautakuwa na athari nyingi za kimazingira kwa sababu utazingatia taratibu za uzalishaji endelevu.

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhandisi Ramo Makani (katikati) akiimba wimbo wa Umoja wa Wafanyakazi (Solidarity Forever) muda mfupi kabla ya kufunga mkutano huo leo terehe 10 Aprili, 2017 pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali Gaudence Milanzi (wa pili kushoto), Mwenyekiti wa Baraza hilo, Esther Malima (wa pili kulia), Mkurugenzi wa Idara ya Wanyamapori, Prof. Alexandre Songorwa (wa kwanza kulia) na Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Rasilimali Watu, Mrimia Mchomvu.

Wakati huo huo, Waziri Maghembe amemuagiza Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania kumuhamisha kituo cha kazi Mkuu wa Kikosi cha Kufuatilia na Kuzuia Uharibifu wa Misitu wa Wakala hiyo, Arjason Mloge kutoka Makao Makuu ya Taasisi hiyo kwenda chuo cha Viwanda vya Misitu (FITI) kilichopo mkoani Kilimanjaro na badala yake atafutwe mtu mwingine muaminifu.

BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...