RAIS
Dk. John Pombe Magufuli anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa
uwekaji wa jiwe la msingi wa ujenzi reli ya kisasa itakayofanyika
kesho Pugu, Ilala jijini Dar es Salaam.
Akizungumza
jijini Dar es Salaam katika sehemu ya uzinduzi huo, Mkuu wa Mkoa wa Dar
es Salaam, Paul Makonda amesema kuwa watanzania waunge mkono jitihada
zinazofanywa na serikali ya awamu ya Tano chini ya Rais Dk. John Pombe
Magufuli.
Amesema reli hiyo ni ya kisasa ambayo itarahisisha usafiri wananchi kuondokana na adha ya kusafiri kwa muda mrefu.Makonda amesema baada ya uzinduzi ajira zitatoka katika ujenzi wa reli hiyo na kuwataka wataopata ajira kuwa walinzi reli hiyo.
Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Reli (TRL) Mhandisi Massanya Kadogosa amesema kuwa ujenzi huo utaanza kwa awamu .Amesema
miundombinu hiyo hiyo ikikamilika gari moshi litatembea kilomita 160
kwa sasa hivyo kwa safari zote zitakuwa ni fupi na wananchi wanaweza
kujenga uchumi.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akioneshwa na Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Sophia Mjema maandalizi ya uzinduzi wa uwekaji wa jiwe la msingi wa reli ya kisasa Standard Gauge Pugu jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akipata maelekezo kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Reli Tanzania (TRL), Mhandisi ,Massanja Madogosa juu ya katika maandalizi ya a uzinduzi wa uwekaji wa jiwe la msingi wa reli ya kisasa Standard Gauge Pugu jijini Dar es Salaam.
.Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akitoa maelekezo kwa watendaji walipotembelea maandalizi ya uzinduzi wa uwekaji wa jiwe la msingi wa reli ya kisasa 'Standard Gauge' kesho Pugu jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Reli Tanzania (TRL) Mhandisi Massanja Kadogosa akizungumza na waandishi wa habari juu ya uzinduzi wa uwekaji wa jiwe la msingi wa reli ya kisasa utaofanyika kesho Pugu jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wananchi waliofika kushuhudia eneo hilo la tukio hapo kesho
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...