Rais Mstaafu na Mjumbe Maalum wa Kamisheni ya Kimataifa ya Kugharamia Fursa za Elimu Duniani Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete amekamilisha ziara yake ya kuhamasisha utekekezaji wa Ripoti ya Kamisheni hiyo ijulikanayo kama 'Kizazi Cha Elimu' (The Learning Generation).
Katika ziara hiyo iliyomfikisha katika nchi 15, Rais Mstaafu Kikwete amekutana na Wakuu wa Nchi 12 wa nchi za Uganda, Malawi, Msumbiji, Congo, Tunisia, Ghana, Chad, Gabon, Ivory Coast, Namibia, Afrika Kusini na Botswana. Aidha amekutana na Makamu wa Rais wa Nigeria na Mawaziri Wakuu wa Ethiopia na Tanzania. Pamoja na viongozi wa nchi na Serikali, Rais Mstaafu amekutana na viongozi wa Taasisi za Kikanda 3  ambao ni Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika (AUC), Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) na Katibu Mtendaji wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC).





Madhumuni ya ziara hizo yalikuwa ni kufikisha ujumbe wa Kamisheni na Ripoti yake juu ya umuhimu wa nchi za uchumi wa kati na chini (low and middle income countries) kufanya mapinduzi makubwa ya elimu ili kukabiliana na janga kubwa la elimu linaloinyemelea dunia. 
Kwa mujibu wa Ripoti ya Kamisheni hiyo, ubora wa elimu inayotolewa na nchi zinazoendelea za uchumi wa kati na chini ni ile ambayo imetolewa na nchi zilizoendelea miaka 70 iliyopita. Aidha, nchi zinazoendelea ziko nyuma sana katika vigezo vitatu muhimu vya elimu vya fursa  ya kujiunga na elimu (access to education), kumaliza elimu (completion) na ufaulu na kuelimika (learning outcomes). 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...