WAZIRI
wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na
Wenye Ulemavu), Mhe. Jenista Mhagama ametoa wito kwa waajiri wote nchini
kujisajili kwenye Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi, (WCF) kama sheria
inavyotaka.
Akizungumza
wakati wa maadhimisho ya siku ya Usalama na Afya Mahali pa kazi duniani
yaliyofanyika Aprili 28,2017 kitaifa katika viwanja vya Chuo Kikuu cha
Ushirika mkoani Kilimanjaro, alisema bado kuna mwamko mdogo kwa waajiri
kujisajili katika Mfuko huo.
“Serikali inathamini sana juhudi zenu kama waajiri katika kuajiri
wafanyakazi, niwaombe sana Chama Cha Waajiri nchini tushirikiane katika
kuongeza hamasa ya kujisajili kwenye Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi ili
hatimaye, Wafanyakazi wenu waweze kupata stahiki (Mafao), zao pindi
wapatwapo na matatizo ya kiafya wanapokuwa kazini,” alisema Waziri
Mhagama.
Kwa
upande wake Mkurugenzi wa Huduma za Matibabu na Tathmini kutoka Mfuko
wa Fidia kwa Wafanyakazi – WCF, Dkt. Abdulssalaam Omary
Alisema
mwitikio mpaka sasa kati ya waajiri 23,000 waliowabaini 700 pekee ndiyo
wamesajiliwa katika mfuko huo hivyo kuiomba serikali isaide kuhamasisha
waajiri wajisajili kwenye mfuko huo.
Katika
hatua nyingine Dkt. Omary alisema katika kipindi cha Mwezi Julai,2016
mpaka Machi 31,2017 wamepokea taarifa ya matukio 478 kutoka kwenye
maeneo ya kazi.
Alisema
kati matukio hayo 478,matukio ya ajali ni 454,magonjwa sita na vifo 18
katika maeneo ya viwandani,migodini na vyombo vya usafiri ambapo
waliopata ajali huduma ya fao la matibabu
Aidha
alisema mfuko huo unatoa mafao 7 ambayo ni mafao ya huduma ya
matibabu,malipo ya ulemavu wa muda,malipo ya ulemavu wa kudumu,malipo ya
anayemhudumia mgonjwa,huduma za ukarabati na ushauri nasaha,huduma za
mazishi na malipo ya wategemezi. Angalia picha za matukio yaliyojiri
katika banda la WCF katika viwanja vya Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi
mkoani Kilimanjaro.
Waziri
wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye
Ulemavu Jenista Mhagama amewataka waajiri nchini kujitokeza kwa wingi
kujisajili katika Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (Workers Compesation
Fund – WCF) kwa ajili ya kuwawezesha waajiriwa kupata mafao pindi
wanapoumia,kuugua au kufariki wakiwa kazini.
Mkuu
wa Kitengo cha Mahusiano WCF, Laura Kunenge akimkaribisha Waziri wa
Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye
Ulemavu Jenista Mhagama katika banda la WCF wakati wa maadhimisho ya
siku ya Usalama na Afya Mahali Pa Kazi mwaka 2017 katika viwanja vya
Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi mkoani Kilimanjaro.
Mkurugenzi
wa Huduma za Matibabu na Tathmini kutoka Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi
– WCF, Dkt. Abdulssalaam Omary akiwasilisha mada fupi kuhusu Mfuko huo
ambapo alisema walengwa wa mafao yanayotolewa na WCF kuwa ni wafanyakazi
wa sekta ya umma na binafsi ambao wataumia au kuugua kutokana na kazi
walizoajiriwa nazo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...